Irani itakapoipiga Israeli, kama ambavyo imeshaahidi, Israeli itajibu
mapigo. Kwa vile Israeli ina nguvu zaidi kuliko Irani, itaipiga Irani
kwa silaha za kawaida. Itaipiga hata kwa silaha za kinyukilia pia.
Kutunisha misuli, Irani itaomba msaada wa kijeshi kutoka katika nchi za
Kiarabu; ambazo zitakubali kuingilia kati na kuisaidia Irani. Kwa
silaha za kawaida, bado nchi zote za Kiarabu zitakazokubali kuisaidia
Irani hazitakuwa na uwezo wa kuishinda Israeli. Kuishinda itabidi
zitumie silaha za kinyukilia.
Silaha za kinyukilia zitakapoanza
kutumika, Marekani itaingilia kati kuisaidia Israeli. Marekani
itakapoingilia kati kuisaidia Israeli, Urusi itaingilia kati kuisaidia
Irani. Ufaransa, Uingereza na Ujerumani zitaingilia kati kuisaidia
Israeli; huku China ikiingilia kati kuisaidia Irani. Hapo Vita Kuu ya
Tatu ya Dunia itaanzishwa rasmi.
Katika vita hiyo ya kinyukilia
na mbaya kuliko vita zote zilizowahi kupiganwa, Israeli itashinda vita
na itaanzisha utawala wa Mpinga Kristo duniani kote. Kutakuwa na dini
moja. Kutakuwa na serikali moja. Kutakuwa na sarafu moja. Watu
watapungua hadi kufikia milioni 500, kama ilivyokuwa mwaka 1650,
asilimia 7 ya idadi ya watu wote ya leo.
Wafuasi wa Yesu Kristo
watapata taabu kubwa ambayo haijawahi kutokea. Yeyote atakayempinga
Mpinga Kristo, yeyote atakayepinga utawala wa Mpinga Kristo, atakiona
cha mtema kuni. Watu wengi watauwawa kwa sababu ya ufuasi wao kwa
Masihi. Wale watakaokuwa na talanta ya kuhubiri watauwawa kinyama,
hadharani, ili liwe fundisho kwa wafuasi wengine wa Yesu Kristo.
Miongoni mwa wale watakaokuwa wanahubiri injili ya kweli ya ufalme wa
Mungu bila woga wa aina yoyote ile, atakuwemo Eliya na Enock. Eliya na
Enock Mungu aliwachukua bila kuonja mauti, kama akiba, kwa sababu ya
kipindi hicho cha Taabu ya Yakobo.
Eliya na Enock wataibuka
ghafla jijini Yerusalemu na kuanza kuhubiri injili ya kumpinga Mpinga
Kristo. Kwa vile hawataogopa chochote, wala hawatamwogopa yeyote,
serikali ya Israeli itawakamata na kuwatesa lakini hawatanyamaza.
Mpinga Kristo atakapoona imeshindikana kuwanyamazisha, Eliya na Enock,
huku akitamba kwamba yeye ndiye Yesu Kristo ambaye kila mtu ndiye
aliyekuwa akimsubiri arudi kwa mara ya pili; na kwamba yeye anatoka
katika ukoo wa mfalme Daudi, ili watu waamini kama kweli yeye ndiye Yesu
Kristo, ataamuru Eliya na Enock wauwawe hadharani kama wahubiri
wengine.
Eliya na Enock watakapouwawa, Mungu atawafufua na
watarudi mbinguni wakiwa wameonja mauti kama binadamu mwingine yeyote
yule. Hapo mlango wa rehema utakuwa umefungwa. Muda wowote kuanzia hapo
Yesu atarudi, kwa mara ya pili, na kwa ajili ya ufufuo wa kwanza.
Watakatifu wote watanyanyuliwa na wataondoka pamoja na Yesu kuelekea
mbinguni, kwa ajili ya ziara ya miaka 1000 katika ulimwengu wa roho;
kuanzia dunia ya kwanza ya ulimwengu huo iitwayo Asiyah hadi ya mwisho
iitwayo Adam Kadmon, katika mji mpya wa Yerusalemu.
Baada ya
milenia, kipindi hicho huku duniani Ibilisi akiwa kifungoni na malaika
wake, binadamu wote wenye dhambi wakiwa wamekufa, Yesu na watakatifu
wote atarudi kwa ajili ya ufufuo wa pili; na kama mfalme wa ulimwengu
wote milele.
Wenye dhambi watafufuliwa na wataungana na Ibilisi
kuipiga Yerusalemu Mpya itakayokuwa inang'inia hewani, huku Yesu na
watakatifu wote wakiwa hawana silaha yoyote; lakini vilevile wakiwa
hawapigwi kwa silaha yoyote.
Shetani atakapoonekana kushindwa,
Yesu atawasha ‘kibiriti cha kiroho’. Mafuta yote yaliyopo ardhini dunia
nzima yatalipuka na kugeuza ardhi yote kuwa ziwa la moto, na hivyo wenye
dhambi wote kupata aibu ya milele.
Katika Biblia kuna tabiri
333 kuhusu maisha ya Yesu Kristo, na kuhusu kurudi kwake kwa mara ya
pili. Kati ya hizo, 332 zilitimia! Bado mmoja tu: Kurudi kwa Yesu Kristo
kwa mara ya pili.
Unadhani huo wa kurudi kwa Yesu Kristo kwa
mara ya pili hautatimia? Muda umefika. Jitathmini katika maisha yako na
uchague lililo jema.
Enock Maregesi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
-
Mercury Cougar ya John Murphy aliyonunua mwaka 1990 kwa gharama kubwa huko Michigan nchini Marekani. Gari hilo lililorekebishwa kwa ajili ...
-
Siku ya kuzaliwa ni siku ya kwanza ya safari nyingine ya siku 365, saa 5, dakika 48, sekunde 46 na maili milioni 600 kulizunguka jua. Safi...
-
41. Ukitaka kuwa mfanyabiashara mzuri wa madawa ya kulevya usitumie madawa ya kulevya. Siri ya mafanikio ya Kolonia Santita ni nidhamu na ...
No comments:
Post a Comment