268. Ukiwa na maarifa utaomba kile unachostahili kupata. Lakini ukiwa huna utaamrisha.
Watu hawajui kuomba ndiyo maana Mungu akasema tushukuru kwa kila jambo, jema au baya, kwa sababu tutabarikiwa kulingana na fadhila na rehema zake.
Watu badala ya kumwomba Mungu wanamwamrisha. Mtumwa hawezi kumshauri bwana wake, sembuse mwanadamu kumwamrisha Mungu?
Mungu anasema katika Isaya 45:11, “Bwana, Mtakatifu wa Israeli, na Muumba wake, asema hivi; Niulize habari za mambo yatakayokuja; mambo ya wana wangu, na habari ya kazi ya mikono yangu; haya! Niagizeni.” Lakini je! Hivyo ndivyo Mungu anavyomaanisha? Kwamba tumwamrishe yeye? Mungu anamaanisha tupeleke shida zetu kwake kwa sababu hakuna mungu mwingine isipokuwa yeye. Kama hatajibu, shida zetu hazitajibiwa.
Kwa sababu Isaya 45:9-10 inasema, “Ole wake ashindanaye na Muumba wake! Kigae kimoja katika vigae vya dunia! Je! Udongo umwambie yeye aufinyangaye; Unafanya nini? Au kazi yako, Hana mikono? Ole wake amwambiaye baba yake, Wazaa nini? Au mwanamke, Una utungu wa nini?”
Unaona? Mungu hawezi kuwa mtumwa, nasi hatuwezi kuwa Mungu. Mungu ataendelea kutuamrisha, nasi kupitia Roho wa Mungu tutaendelea kuomba kile Mungu alichopanga tupate.
Watu hawajui kuomba ndiyo maana Mungu akasema tushukuru kwa kila jambo, jema au baya, kwa sababu tutabarikiwa kulingana na fadhila na rehema zake.
Watu badala ya kumwomba Mungu wanamwamrisha. Mtumwa hawezi kumshauri bwana wake, sembuse mwanadamu kumwamrisha Mungu?
Mungu anasema katika Isaya 45:11, “Bwana, Mtakatifu wa Israeli, na Muumba wake, asema hivi; Niulize habari za mambo yatakayokuja; mambo ya wana wangu, na habari ya kazi ya mikono yangu; haya! Niagizeni.” Lakini je! Hivyo ndivyo Mungu anavyomaanisha? Kwamba tumwamrishe yeye? Mungu anamaanisha tupeleke shida zetu kwake kwa sababu hakuna mungu mwingine isipokuwa yeye. Kama hatajibu, shida zetu hazitajibiwa.
Kwa sababu Isaya 45:9-10 inasema, “Ole wake ashindanaye na Muumba wake! Kigae kimoja katika vigae vya dunia! Je! Udongo umwambie yeye aufinyangaye; Unafanya nini? Au kazi yako, Hana mikono? Ole wake amwambiaye baba yake, Wazaa nini? Au mwanamke, Una utungu wa nini?”
Unaona? Mungu hawezi kuwa mtumwa, nasi hatuwezi kuwa Mungu. Mungu ataendelea kutuamrisha, nasi kupitia Roho wa Mungu tutaendelea kuomba kile Mungu alichopanga tupate.
No comments:
Post a Comment