Friday 15 June 2018

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu.

Kila mtu kabla ya kuzaliwa roho yake iliumbwa na Mwenyezi Mungu na kupangiwa nchi itakapozaliwa na kuishi. Katika nchi hiyo Mungu akatanguliza malaika mwema ambaye kazi yake ni kumsaidia mtu mwenye roho hiyo tangu kuzaliwa kwake hadi kufa kwake hadi baada ya hapo.

Lakini Shetani atakapoinasa roho hiyo, kabla mwenye nayo hajazaliwa, ataibadilisha ili izaliwe sehemu nyingine tofauti na pale alipopanga Mungu; ili imtumikie yeye badala ya kumtumikia Mungu.

Kujua uraia halisi wa roho yako, hivyo kuujua uraia wako, lazima ujitambue; lazima ujue kwa nini ulizaliwa.

Mungu akikuweka mahali unapostahili kuwa, kulingana na takdiri ya maisha yako, hakuna mtu mwenye uwezo wa kushindana na kipaji chako.

Ishi mahali unapostahili kuishi.

No comments:

Post a Comment

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...