Monday 5 March 2018

Hakuna Magonjwa

267. Hakuna magonjwa. Magonjwa yote yamo akilini mwetu. Ukitaka kulithibitisha hilo nenda hospitali yoyote ya Dar kisha toa tangazo la sauti kwamba Al-Shabaab wako nje watalipua jengo zima kwa mabomu. Asilimia 95 ya hao unaosema ni wagonjwa watakimbia hadi Bagamoyo.

Uongo wa daktari ni ukweli wa mgonjwa. Wakati mwingine maneno mazuri na huduma nzuri humponyesha mgonjwa. Kataa magonjwa yote kwa damu na jina la Yesu.

Tunaona magonjwa nje, nje ya akili zetu, ili tuone ni wapi tumekosea, ili tujirekebishe kwa ndani.

Magonjwa yote tunayoyaona watu wakiugua au sisi wenyewe tukiugua yako ndani ya akili zetu. Tunayaona nje, ya akili zetu, ili tuwe na uhusiano na magonjwa hayo, kusudi tuone ni wapi tumekosea, ili tujirekebishe kwa ndani. Kwa hiyo kama mtu anaumwa malaria ujue ndani ya akili yako kwamba malaria ni ugonjwa mbaya, na ujirekebishe kwa maana ya kujikinga na mbu wanaosababisha malaria. Hiyo ndiyo asili yetu. Hivyo ndivyo Mungu alivyotuumba na alituumba hivyo kwa manufaa yetu.

Ukiona mtu anaumwa au wewe mwenyewe unaumwa ujue ni ujumbe kutoka ndani unaokusihi ubadilike, uwe kama Mungu anavyotaka uwe.

No comments:

Post a Comment

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...