Miwani ya kipelelezi aina ya Aviator (MicroSD, 32GB, GLSun720P) – 
iliyotumiwa na makachero wa kike wa Kolonia Santita Giovanna Garcia, 
Delfina Moore, Amalia Gonzalez, Mandi Santana na Kamanda wa Makachero wa
 Kolonia Santita Sonia Padilla; kuwapeleleza Vijana wa Tume wa Executive
 Action Corps John Murphy, Radia Hosni, Daniel Yehuda na Frederik 
Mogens; Oktoba, 1992. 
Kamishna Profesa Randall Ortega ndiye aliyekuwa wa kwanza kufika katika Uwanja wa Ndege wa Copenhagen Kastrup, kabla
 ya makamishna wengine. Ndege yake, Lufthansa, iliondoka saa 2:40 usiku 
kwenda Mexico City kupitia Dusseldorf na Frankhurt, Ujerumani. Murillo 
Montana alifika uwanjani hapo mapema na kuondoka saa 4:00 usiku na BA 
kwenda London, Miami, Lima, na Bolivia – mwisho wa safari yake. Wote, 
Ortega na Montana, ndani ya ndege zao, walikaa na wasichana warembo 
waliokuwa na safari sawa na za makamishna. Mmoja, aliyekaa na Ortega, 
alikuwa na safari ya Mexico City kupitia Dusseldorf na Frankfurt, 
Ujerumani – kama Kamishna Ortega. Na mwingine, aliyekaa na Montana, 
alikuwa na safari ya La Paz, Bolivia; kupitia London, Miami na Lima, 
Peru – kama Kamishna Montana. Wasichana hao walikuwa wakarimu, wazuri, 
wacheshi na wapenda watu – wote walivaa miwani myeusi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
- 
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
 - 
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
 

Si kila king'aacho ni dhahabu!
ReplyDelete