D'Angleterre. Hoteli ya kimataifa daraja la kwanza, ‘The grand old of
 the city’, nyota tano, katika kona ya mitaa ya Østergade na Kongens 
Nytorv katikati ya Copenhagen, mkabala na duka kubwa la kujihudumia 
mwenyewe la Magasin du Nord, Radia Hosni, mpelelezi wa Tume ya Dunia 
kutoka Tunisia alipofikia.
Hoteli ya D’Angletere, karibu na sanamu
 la farasi la Mfalme Christian wa Nne na mkabala na duka la Magasin, 
katikati ya geti la mashariki la Copenhagen na Bandari ya Nyhavn, ndipo 
Tume ya Dunia ilipoandaa malazi ya siri ya mpelelezi wake mashuhuri 
Radia Hosni. Lakini, ndani ya saa moja tu, Kolonia Santita wakajua Hosni
 alipokuwa; na kuandaa njama kamambe za kumuua usiku huo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
- 
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
 - 
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
 

No comments:
Post a Comment