Wauzaji
 wadogowadogo wa methi – ‘Pet dealers’ – inayojulikana kwa majina ya 
mtaani kama ‘crank’, ‘crystal’, ‘glass’, ‘hielo’, ‘tik’ au ‘ice’, huuza 
madawa mitaani kwa ajili ya viongozi wa magenge yao. Ukifanya kazi yako 
vizuri unaweza kupanda cheo kutoka muuzaji wa mtaani mpaka msafirishaji 
wa kimataifa. Ukishakuwa msafirishaji wa kimataifa, unaweza kwenda 
Meksiko na kufanya biashara na mamafia wa mashirika ya madawa ya kulevya
 ya huko wewe binafsi. Unaweka oda na kutuma pesa kwenda Meksiko, ambako
 mamafia hupika methi kwa ajili yako, katika maabara kubwa za methi za 
mafichoni. Unaweza kulipa Tsh. 76,500,000 kwa kilo 6 za methi. Oda ya 
kilo 6 ina thamani ya mtaani ya Tsh. 810,000,000. Mamafia husafirisha 
methi kutoka porini hadi kwenye mpaka wa California na Meksiko, ambako 
wasafirishaji huipokea na kuvuka mpaka kuingia Amerika. 
San
 Ysidro (San Sidro, hadithi ya Kolonia Santita ilipoanzia) ni eneo 
lililoko katikati ya Tijuana, Meksiko na San Diego, California. Hapo 
kuna mpaka mkubwa na wenye mishughuliko mingi kuliko yote ya kimataifa 
duniani; na ni eneo ambalo Marekani imelipa kipaumbele kikubwa katika 
vita yake dhidi ya madawa ya kulevya. 
Wasafirishaji
 mara nyingi huwa na magari yenye vyumba vingi vya siri. Wana njia 
nyingi za kuondoa harufu ya madawa ili mbwa wa kipolisi wasiyanuse. 
Vyumba vya siri huweza kuzibwa kabisa (‘vacuum sealed’) kuondoa harufu 
ya madawa ilimradi mbwa wasinuse chochote. 
Wanaposubiri
 kwenye foleni za magari kwa masaa mengi, wasafirishaji hukatisha mpaka 
na kuelekea kwenye maghala kadha wa kadha ya madawa ya kulevya (‘stash 
houses’) katika Jimbo la California. Wanapofika katika majumba yao 
(baada ya kutoka kwenye maghala) mara nyingi wasafirishaji hao 
huchanganya methi na kitu kinaitwa SMS, ambacho ni chakula cha farasi. 
Ukichanganya gramu 227 za SMS utapata asilimia 50 ya methi, yaani 
iliyochanganywa, na kuwadanganya wateja kama ni methamfetamini safi 
isiyokuwa na doa. 
Methi
 hununulika sana. Kadiri ilivyoingia (kwa maana ya uharaka) ndivyo 
itakavyotoka. Wasafirishaji hutakiwa kubeba mzigo wa kutosha wa hata 
wiki nzima, kukidhi mahitaji ya wateja; labda kilo 2 mpaka 5 hivi. 
Wasafirishaji hao wakati mwingine wanaweza kuuza hata kilo 25 mpaka 40 
kwa mwezi kulingana na jinsi watakavyokwepana na vyombo vya dola. 
Katika
 maabara za methi kule Meksiko kuna madumu makubwa ya bluu yenye 
mifuniko myeusi. Hapo wafanyakazi wa mamafia hubadilisha kemikali za 
kutengenezea methi (‘ephedrine’ na ‘pseudoephedrine’) katika chapa ya 
kwao wenyewe, na kuiuza kama Methi au Glasi ya Meksiko nchini Marekani 
na duniani kwa jumla. Mfanyabiashara mmoja wa methamfetamini huweza 
kujiingizia kipato cha mpaka Tsh. 80,000,000 kwa wiki. 
Mamafia
 huzalisha takriban tani 200 za methamfetamini kwa soko la Marekani 
pekee kila mwaka, zenye mapato ya makadirio ya Tsh. 14,000,000,000,000 
(trilioni 14). Biashara ya methi ya Meksiko hutegemea sana mamia ya 
wafanyabiashara na wasafirishaji wa madawa ya kulevya wa mataifa 
mengine. Kukidhi haja ya matakwa hayo kunahitajika uingizaji wa kiwango 
cha juu wa viambato vya kikemikali (‘chemical ingredients’). 
Kupata
 kemikali hizi tangulizi (‘precursors’), mamafia wa Meksiko husafiri 
mpaka Asia ambako ndiko kuna chanzo kikuu cha ‘ephedrine’ na 
‘pseudoephedrine’. China na India, baadhi ya viwanda vya madawa 
huzalisha maelfu ya tani za ‘pseudoephedrine’ kwa ajili ya matumizi 
halali. Walanguzi wa kimafia (‘criminal middlemen’) hununua kihalali 
kiasi kikubwa cha kemikali hizi, na kuziuza baadaye kwa wazalishaji 
haramu wa methamfetamini huko Meksiko na sehemu zinginezo. Barani Asia 
kilo moja ya ‘pseudoephedrine’ huuzwa kwa Tsh. 110,210.70, lakini 
mashirika ya kihalifu ya kimataifa kama mamafia wa Meksiko hulipa mpaka 
kiasi cha Tsh. 16,000,000 kwa hiyo kilo moja. 
Kemikali
 za ‘pseudoephedrine’ hutumwa kutoka huko Asia mpaka katika maabara 
kubwa dunia nzima; ambako hupikwa na kutengeneza methamfetamini, na 
kisha kusambazwa katika maeneo yote ya nchi husika. Biashara hii 
uhudumia takriban watumiaji milioni 51 duniani kote. 
Methi
 huweza kutengenezwa nyumbani. Mbolea ya amonia (‘ammonium fertilizer’) 
na lithi (‘lithium’), kutoka ndani ya betri za kawaida kwa mfano, 
huwekwa ndani ya chupa ya kawaida ya soda na kufunikwa. Kemikali 
zinapofanya kazi hutoa si tu methi, lakini pia fukizo (‘fumes’); lakini 
ambazo zina uwezo wa kulipuka. 
Methi
 ni tofauti na kokeini kwa sababu inaunguza. Humfanya mtumiaji ajisikie 
raha ya kupindukia, nguvu, na makini! Mtumiaji huweza kukaa kwa masaa 
ishirini na nne kwa siku, anaweza kufanya kazi kwa wiki nzima, au wiki 
mbili, bila kupumzika. 
Methi
 huvutwa kwa kutumia buruma (‘pipe’) inayomlewesha mtumiaji kwa haraka 
na vizuri zaidi. Matokeo mabaya ya baadaye ya utumiaji wa dawa hii ya 
ajabu ni pamoja na matatizo makubwa ya afya ya akili, na ukosefu kabisa 
wa hamu ya kula na kulala. Unaweza kujisikia kama vile unataka kuurarua 
uso wako wote! Kujikinga na dalili za namna hiyo, waathirika hulazimika 
kuvuta methi zaidi. Kukosa usingizi ni kubaya. Ukizidi kukaa kwa muda 
mrefu bila kulala, mwishowe utaugua ugonjwa unaitwa ‘matatizo ya akili 
ya wasiwasi’ (‘severe paranoid psychosis’). 
Kama
 heroini, ukitumia methi utajisikia raha ya kupindukia. Kawaida, watu 
huanza kuvuta methi baada tu ya saa sita za usiku; utataka buruma 
nyingine, utataka tena kujidunga. Kisha utafanya vitu vya ajabu kama 
kusafisha nyumba mpaka asubuhi na kadhalika. Dozi kubwa ya methi huweza 
kusababisha kiharusi, maruweruwe, ugonjwa wa moyo, na kifo. 
Ndani
 ya methi kuna kemikali yenye nguvu sana iitwayo LSD (‘Lysergic acid 
diethylamide’) inayohusika na maono yote ya kiwendawazimu. Maono ya 
kiwendawazimu (‘hallucinations’) yanayosababishwa na LSD ya methi 
huonekana kama taswira za kweli kabisa! Kadiri akili inavyoathirika 
ndivyo hata mwili unavyoathirika pia. 
Dalili
 kubwa ya waziwazi ya methi ni ugonjwa ujulikanao kama ‘mdomo wa methi’ 
(au ‘meth mouth’), ambapo waathirika huonekana wakijing’ata meno yao 
wenyewe. Kemikali za ndani ya dawa hiyo hutafuna meno na fizi; na tezi 
za mate hukauka mdomoni. Zote hizi husababisha meno kuchakaa na kuoza; 
na mwishowe kupotea mdomoni. Waathirika wa muda mrefu hujikuta pia 
wakiwa waoga kupita kiasi na wagomvi, hivyo vurugu majumbani mwao 
kuongezeka. 
Methi
 husababisha ubongo ufungulie vitarishi vya kikemikali viitwavyo ‘neural
 transmitters’ ambavyo hutufanya tunuke, tuhisi, na tuishi kulingana na 
mazingira fulani. Mojawapo ya vitarishi hivyo, ambavyo kimsingi 
huathiriwa na methi, ni ‘dopamine’. ‘Dopamine’ hujulikana kama kitarishi
 cha furaha. Madawa mengi ya kulevya huamsha mtiririko wa ‘dopamine’ 
kwenye ubongo, lakini methi hufurisha ubongo kwa kiasi cha hadi asilimia
 1200 cha ‘dopamine’, kuliko ilivyo kawaida. Kuna mafuriko makubwa ya 
‘dopamine’ yanayofanya mtu ajisikie raha kubwa ya kupindukia; na ambayo 
pia humfanya mtumiaji ajisikie kama mtu hodari wa kupindukia. 
Lakini
 sehemu zote za ubongo zinazopokea meseji hizi (‘dopamine receptors’) 
uharibiwa na sumu iliyomo ndani ya methi. Mtu akiendelea kutumia methi 
kwa muda mrefu, hivi vyumba (‘receptors’) husimama kufanya kazi. 
Waathirika wa methi huweza kuwa na ‘dopamine receptors’ chache (kwa hadi
 asilimia 16) kulinganisha na ubongo wa kawaida wa mtu asiyetumia 
madawa. 
Waathirika
 wa methi hawana uwezo wa kujidhibiti wenyewe. Wanaweza kukosa mchocheo 
(au ‘impulse’) wa kuiba, kwa mfano. Yaani wanaweza kuona kuiba ni jambo 
la kawaida, si kosa la kumpeleka mtu jela. Hupatiwa huduma ya saikolojia
 ya kimatibabu kwa ajili ya matumizi mabaya ya madawa ya kulevya – 
mchanganyiko wa maandiko mbalimbali ya kujisomea, vipindi vya matibabu 
vya kimakundi, na ushauri nasaha kwa kila mmojawao. Hawafanyi kazi, 
hawachangii chochote katika chumi za nchi zao. Methi huathiri moja kwa 
moja kituo kikuu cha furaha cha ndani ya vichwa vyao. 
Methi
 ni dawa inayotumiwa (‘abused’) vibaya kuliko yote duniani. Ni dawa 
hatari kutengeneza, na ni dawa hatari kutumia. Methi hujulikana katika 
vyombo vya dola kama tatizo namba moja la madawa ya kulevya duniani; kwa
 sababu huwafanya watu washindwe kabisa kujizuia. 
Vidonge
 vya mafua na aleji vina ‘pseudoephedrine’ ndani yake. Wafamasia hudai 
kuwa asilimia 80 ya mauzo yote ya ‘pseudoephedrine’ huenda kwenye 
uzalishaji wa methi. Vidonge vya Tsh. 8,000 huweza kuzalisha methi ya 
Tsh. 80,000. Kila gramu ina thamani ya Tsh. 162,000, ambayo ni kubwa 
kuliko kokeini au heroini. 
Kuvuta
 heroini kwa kutumia karatasi ya aluminiamu au balbu au kiko cha kioo au
 kwenye kijiko, huitwa ‘chasing the dragon’. Kuvuta methamfetamini 
huitwa ‘chasing the white dragon’. Usimfukuze nyoka, hutampata.

No comments:
Post a Comment