Saturday 31 December 2016

Kikamilikacho si Kiimarishwacho

Kikamilikacho si kiimarishwacho. Rais wa Tume ya Dunia alilazimishwa, kufanya kazi aliyokuwa amejitolea maisha yake yote kuipigania kwa nguvu zake zote, na utendaji wake mzuri wa kazi uliharibika.

Kitu kikishakamilika hakiwezi tena kuimarishwa ukilazimisha utakiharibu. Rais wa Tume ya Dunia, Boidin Tony Versnick, alitishwa na Umoja wa Mataifa kuondolewa katika wadhifa wake iwapo angeshindwa kumkamata Panthera Tigrisi ndani ya siku saba bila kujali uaminifu, uthabiti, uvumilivu, uadilifu na uchapakazi wake hodari katika Tume ya Dunia. Mbali na ukamilifu huo katika kazi hata hivyo, kilichokamilika kililazimika kuimarishwa. Versnick ndani ya hizo siku saba alipigana kufa na kupona kutetea wadhifa wake, thamani yake ya utu na kujitengenezea nafasi nzuri katika historia ya Tume ya Dunia na ya Umoja wa Mataifa na ya dunia kwa jumla. Hakuzijali tena sifa zake za kazi, hakujali sheria, hakujali vitisho vya Umoja wa Mataifa. Lakini pamoja na kazi nzuri aliyofanya, Boidin Versnick alilazimika kujiuzuru wadhifa wake; nafasi yake ikachukuliwa na Makamu wa Rais wa Tume ya Dunia, Jørgen Vestergaard Laursen, aliyekuwa na umri wa miaka sitini na mchapakazi hodari kutoka Denmaki. Versnick alipigana na Kolonia Santita kwa pupa, licha ya shinikizo la Umoja wa Mataifa. Usimlazimishe mtu kufanya kazi ambayo tayari anaifanya vizuri.

No comments:

Post a Comment

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...