Kila mtu kabla ya kuzaliwa alipewa na Mwenyezi Mungu unabii na nyota
ya ufalme. Una bahari ya fursa ya kuwa kitu chochote unachotaka kuwa
katika dunia hii. Kama unataka furaha, furaha iko ndani yako. Kama
unataka utajiri, utajiri uko ndani yako. Kama unataka amani, amani iko
ndaniyako. Kama wewe ni tone na fursa ni bahari, wewe ni bahari ndani
ya tone.
Unabii ni uwezo alionao mtu wa kuongea mambo matakatifu
ya Mungu, kuwaongoza wenzake katika njia njema. Mungu humwambia nabii
kitu cha kusema na nabii huwambia wenzake kile ambacho Mungu amemwambia
aseme. Mungu hawezi kuongea na watu mpaka watu wajue jinsi ya kuongea
naye, na wakati mwingine ni rahisi sana kusikia ujumbe kutoka kwa mtu
kuliko kuusikia ujumbe huo moja kwa moja kutoka kwa Mungu. Mungu anaweza
kukwambia useme kitu fulani kwa mtu au watu fulani. Unaweza usijue kwa
nini anakwambia ufanye hivyo, lakini utajisikia msukumo wa hali ya juu
wa kutangaza ujumbe uliopewa kuuwasilisha. Mungu hatakulazimisha, lakini
atakung’ang’aniza, na ni Mungu pekee anayejua lengo la mawasiliano
hayo. Mungu akikwambia ufanye kitu fanya mara moja, usiulize kwa nini.
Kazi yako ni kufanya unachotakiwa kufanya, kusema unachotakiwa kusema,
si kuuliza maswali. Mtumie rafiki yako wa kiroho kukuongoza katika mema
na mabaya, na usitambe – kwamba unaongea maneno uliyoambiwa na Mungu
uyaongee. Ukiwa na uwezo mkubwa wa kuongea na Mungu utaleta mabadiliko
katika dunia.
Mungu humwambia mtu kitu cha kusema na mtu huwambia
wenzake kile ambacho Mungu amemwambia aseme. Lakini utajuaje kama Mungu
amekuchagua wewe kusema au kufanya kitu? Mungu atakwambia kupitia Roho
Mtakatifu, na utajisikia msukumo mkubwa wa kusema au kufanya kile
ambacho Mungu anataka useme au ufanye. Unabii unaweza kumtokea mtu
yoyote, mahali popote, anayejua jinsi ya kuwasiliana na Mungu.
Nyota
ni kipaji, kipawa, takdiri, karama, au uweza; ni kiashiria cha rohoni
kinachoonyesha mtu atakuwa nani baadaye, mafanikio ya mtu, au takdiri ya
maisha ya mwanadamu. Unabii na nyota ya ufalme ni kibali cha Mungu
katika maisha ya mtu. Kupata kibali hicho, tembea na watu sahihi katika
maisha yako (tembea na watu ambao Mungu amekuchagulia kushika funguo za
takdiri ya maisha yako). Tamka na kukiri kibali cha Mungu katika maisha
yako yote. Panda mbegu za kibali cha Mungu katika udongo wa maisha yako.
Jifunze kutenda mema bila malipo, kwani wema ni mbegu ya kibali cha
Mungu. Jali mambo ya ufalme wa Mungu.
Wengine hatuishi kama
wafalme kwa sababu ya nguvu za giza – zilizopo kati ya Mungu na
wanadamu. Nyota zetu zimefunikwa. Una kila kitu unachotafuta, ndani ya
moyo wako. Usitafute furaha, utajiri au amani nje ya moyo wako. Tafuta
furaha, utajiri au amani ndani ya moyo wako.
Kila mtu ana karama yake mwenyewe itokayo kwa Mungu.
ReplyDeleteUna kifurushi cha fursa ndani ya moyo wako, kitakachokuwezesha kuishi maisha yoyote utakayoyataka katika dunia hii.
ReplyDeleteTayari Mungu ameshakufadhili. Tafuta kibali chake uishi kama anavyotaka. Kibali cha Mungu ndiyo mtaji wa maisha yako.
ReplyDelete