Hellerup, Copenhagen, Denmaki, kitongoji cha matajiri wa Copenhagen 
katika pwani ya ukanda wa bahari wenye hadhi ya kimataifa ya Bendera ya 
Bluu wa Øresund (Sound, Sauti) ukanda wa bahari unaotenganisha kisiwa 
cha Denmaki cha Sjælland (Zealand, Copenhagen) na jimbo la Swideni la 
Skåne (Scania, Malmö), Barabara ya Strandvejen, Kaskazini ya ‘Indre By’,
 katika nyumba ya mpelelezi wa Tume ya Dunia aliyefundishwa na makomandoo wa SAS wa Uingereza Frederik Morgens. 
 
 Mpelelezi wa Tume ya Dunia Frederik Mogens ana nyumba mbili katika jiji
 la Copenhagen. Moja iko kaskazini-magharibi mwa Copenhagen katika 
kitongoji cha Norrebro; na nyingine Hellerup, kaskazini mwa Copenhagen. 
Norrebro ni nyumba yake rasmi ya familia aliyojenga yeye, wakati 
Hellerup ni nyumba yake ya siri aliyojengewa na Tume ya Dunia. Nyumba ya
 siri ya Mogens ni nyumba ya kisasa yenye mandhari nzuri ya kuvutia hasa
 sebuleni; kulikonakshiwa kwa televisheni na simu, jokofu dogo, mapambo 
ya wanyama, michoro ya rangi ya wasanii wa kale kama Pablo Picasso na 
Christoffer Eckersberg, na makochi makubwa ya Hans Wegner. Mipango yote 
ya Operesheni Kimbunga ilifanyika katika nyumba hiyo ya ghorofa: kabla 
ya Vijana wa Tume kwenda Roskilde (uwanja wa ndege wa Copenhagen) 
kupanda Grumman ya tume, kuelekea Guadalajara nchini Meksiko.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
- 
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
 - 
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
 

Hapo ndipo ilipo nyumba ya siri ya mpelelezi wa Tume ya Dunia Sajini Frederik Mogens kutoka Denmaki.
ReplyDelete