Eneo la kihistoria la mjini Tunis nchini Tunisia linalosifika kwa
majengo mengi ya kale na mitaa mingi myembamba iliyoshonana, Medina,
Mpelelezi wa Tume ya Dunia Radia Hosni alipomshusha mchumba wake Fathi
Meoki – kipindi akielekea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Carthage (kutokea Uwanja wa Mpira wa El-Manzeh) kumpokea Bosi wa Kanda
ya Afrika ya Kaskazini ya Tume ya Dunia Hussein Kashoggi.
Ijumaa,
Radia alikuwa na ratiba ya kumpokea Hussein Kashoggi katika Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Carthage na kumshusha Meoki, Fathi Meoki, mchumba
wake, huko Medina, madukani. Meoki, 40, alitaka kununua zulia na vitu
vingine vya ndani kwa ajili ya nyumba yao mpya, halafu Radia angempitia
baadaye – baada ya kumshusha kamishna. Walivyotoka El-Manzeh, Radia na
Meoki (wote warefu) walijitupa ndani Quadrifoglio (Alfa Romeo) nyeupe na
kuondoka mpaka Barabara ya Ufaransa, mwanzoni mwa Place de la Victoire
na ‘Bab el Bahar’ (lango la Medina), mkabala na Ubalozi wa Uingereza,
ambako Meoki alishuka na kuingia madukani. Radia kisha akaendesha gari
lake mpaka Carthage, nje ya mji, ambako pia ndiko alikoishi (yeye na
shangazi yake) kumpokea kamishna saa 9:40 adhuhuri.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
-
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
-
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
-
Uwanja wa Ndege wa Copenhagen-Roskilde: uliotumiwa na Tume ya Dunia na Kolonia Santita kwa pamoja – kilometa tisa kutoka katika Kanisa ...

No comments:
Post a Comment