Eneo la kihistoria la mjini Tunis nchini Tunisia linalosifika kwa 
majengo mengi ya kale na mitaa mingi myembamba iliyoshonana, Medina, 
Mpelelezi wa Tume ya Dunia Radia Hosni alipomshusha mchumba wake Fathi 
Meoki – kipindi akielekea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa 
Carthage (kutokea Uwanja wa Mpira wa El-Manzeh) kumpokea Bosi wa Kanda 
ya Afrika ya Kaskazini ya Tume ya Dunia Hussein Kashoggi.
Ijumaa, 
Radia alikuwa na ratiba ya kumpokea Hussein Kashoggi katika Uwanja wa 
Ndege wa Kimataifa wa Carthage na kumshusha Meoki, Fathi Meoki, mchumba 
wake, huko Medina, madukani. Meoki, 40, alitaka kununua zulia na vitu 
vingine vya ndani kwa ajili ya nyumba yao mpya, halafu Radia angempitia 
baadaye – baada ya kumshusha kamishna. Walivyotoka El-Manzeh, Radia na 
Meoki (wote warefu) walijitupa ndani Quadrifoglio (Alfa Romeo) nyeupe na
 kuondoka mpaka Barabara ya Ufaransa, mwanzoni mwa Place de la Victoire 
na ‘Bab el Bahar’ (lango la Medina), mkabala na Ubalozi wa Uingereza, 
ambako Meoki alishuka na kuingia madukani. Radia kisha akaendesha gari 
lake mpaka Carthage, nje ya mji, ambako pia ndiko alikoishi (yeye na 
shangazi yake) kumpokea  kamishna saa 9:40 adhuhuri.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
- 
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
 - 
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
 

No comments:
Post a Comment