200. Mungu akikubariki kipaji chako watu watasema ni laana. Maisha yako
ni sawa na mto. Unakoelekea ni baharini. Lakini sasa umefika kwenye
mlango wa bahari. Unahangaika upite wapi kufika baharini, ambapo
utaogelea kwa kadiri utakavyoweza. Utakapofika baharini, watu, badala ya
kusema umebarikiwa, watasema umelaaniwa, badala ya kukuita malaika,
watakuita shetani. Mafanikio hayapimwi kwa pesa au mali kiasi gani
unayo, mafanikio yanapimwa kwa amani ya moyo au maisha ya watu kiasi
gani umeboresha.
Unapofikia hatua ya kuwa na kila kitu katika maisha, unapokuwa
umefanya kila kitu ulichotamani kufanya katika maisha, unakuwa na bahari
nzima ndani ya tone ambalo ni wewe. Unaridhika. Wewe si tone tena ndani
ya bahari, wewe ni bahari ndani ya tone. Kinachobaki baada ya hapo ni
kusaidia jamii iliyosaidia kukulea ulipokuwa mdogo, kuacha alama katika
dunia kabla na baada ya wewe kuondoka, bila kujali watu watasema nini
juu ya maisha yako.
Boresha maisha ya watu kwa kadiri
utakavyoweza. Ukisaidia mtu 1 watahurumiwa watu 10. Ukisaidia watu 10
watahurumiwa watu 100. Ukisaidia watu 100 watahurumiwa watu 1000. Kila
mmoja wetu akitambua wajibu wake katika jamii, Mungu atatuhurumia sisi
wote. Maisha ya mtu mmoja yakiboreka, mmoja huyo ataboresha na ya
wengine wengi. Hivyo, endelea kuogelea lakini usisahau kurudi nyuma
katika jamii.
http://www.facebook.com/koloniasantita
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
-
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
-
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
-
Uwanja wa Ndege wa Copenhagen-Roskilde: uliotumiwa na Tume ya Dunia na Kolonia Santita kwa pamoja – kilometa tisa kutoka katika Kanisa ...

Amani ya moyo ndicho kipimo cha mafanikio yetu.
ReplyDelete