Monday, 19 May 2014

Kuambiana

Adam Kuambiana umerudi nyumbani ulikotoka, ukiongozwa na imani na mwanga wa wale uliowapenda na kuwapoteza. Hatuwezi kukumbuka kwamba umetutoka bila kukumbuka kwamba uliishi, na kwamba maisha yako yalitupa kumbukumbu nzuri tusizoweza kuzisahau haraka. Jumanne, siku ya kuuaga mwili uliokuwa ukitumiwa na wewe, wengine watasema Kwa heri lakini mimi nitasema Asante! Asante kwa sababu ya kipaji chako. Asante kwa sababu ya kujitahidi kwa kadiri ya uwezo wako wote, kutoa sauti kwa wale wote waliokuwa hawawezi kusikika. Asante kwa sababu ya kuacha dunia katika hali nzuri kuliko ulivyoikuta wakati ukiingia, na Asante kwa sababu ya maisha yako. Tukiendelea kuomboleza kifo cha Adam Kuambiana hapa duniani, wengine wanasherehekea kukutana naye huko mbinguni. Mchungaji wa uhai wa wote Mungu wa mbinguni ailaze roho yake mahali pema peponi: Yeye ni mwandishi wa hadithi ya maisha yetu na ndiye aliyeandika ukurasa wa mwisho wa hadithi ya Adam.

http://www.facebook.com/koloniasantita

3 comments:

  1. Maisha ya watu yamebadilika kwa sababu Adam Kuambiana alikuwepo hapa.

    ReplyDelete
  2. May God Bless Adam Kuambiana, and may he rest in eternal peace.

    ReplyDelete

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...