Monday 4 June 2018

Tumejaa Ulaghai, Unafiki, na Utata

280. Mamilioni ya watu wamechepuka katika mahusiano yao. Wengine wameua na imebaki kuwa siri yao. Wengi wanakwepa kodi ya serikali na hawakamatwi. Lakini hatuwezi kumdanganya Mungu. Kwa sababu anatujua hadi ndani ya mioyo yetu.

Mioyo yetu wenyewe hutudanganya kidogokidogo katika kutenda dhambi, wakati mwingine bila sisi wenyewe kujua. Lakini, iamini Biblia, Mungu hawezi kuichukulia dhambi kirahisirahisi! Kwa sababu anaupenda sana uumbaji wake.

Kuna kitu kibaya sana ndani ya mtu. Hilo liko wazi. Biblia inasema chanzo cha matatizo ya mtu ni moyo wake, roho yake, pamoja na uwezo wake wa kufikiri. Tumejaa ulaghai, unafiki na utata. Tunajichezea sisi wenyewe ule mchezo wa kitoto wa kombolela. Yaani, tunajificha na kujitafuta wenyewe, tunawadanganya watu lakini Mungu anatuona.

Labda ni katika mazingira hayo ambapo moyo hufanya kazi yake kwa uharibifu zaidi. Huficha uovu mkubwa wa dhambi unaoendelea kuwa mkubwa, na matokeo yake kuwa mabaya na mazito zaidi. Moyo unatulaghai katika kufikiri kuwa si mbaya, au kwamba Mungu ni mwenye huruma sana kiasi kwamba atapuuza.

Tusipoacha kutenda dhambi, dhambi haitakomeshwa. Ni wajibu wa kila mmoja wetu kukomesha dhambi katika maisha yake. Usisubiri wengine waikomeshe kabla au kwa niaba yako. Hata serikali haitaweza kukusaidia.

Kuna namna moja tu ya kukomesha dhambi, nayo ni kufunga milango yote ya dhambi baada ya kumkaribisha Mungu katika maisha yako.

Funga milango yako yote ya dhambi na kaa mbali na nyavu zinazowinda watu kabla miguu yako haijanaswa na nyavu hizo.

No comments:

Post a Comment

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...