Monday 28 May 2018

Asili na Fasili

279. Mtu aliyepoteza kila kitu katika maisha yake hana asili wala fasili. Kuwa makini naye. Ana uwezo wa kufanya chochote.

Mtu asiyekuwa na asili wala fasili ni yule asiyekuwa na wazazi wala watoto wala chochote kile katika maisha yake. Si wa kuchezea.

Ujinga ni kutoijua karama yako. Laiti mtu angeijua karama yake angekuwa na kila kitu katika maisha yake.

Ukiijua karama yako utajua kuwa kifo si adui aliyeshindikana, hivyo hakitakusumbua, na utaishi kulingana na kadari ya maisha yako, ukiwa na kila kitu katika maisha.

Kuwa makini na mtu aliyepoteza kila kitu katika maisha yake. Kwa vile hana kitu cha kupoteza, hataona shida kukupoteza.

No comments:

Post a Comment

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...