Friday 15 June 2018

Maisha Mkebe wa Hesabu

284. Maisha ni kama mkebe wa hesabu. Ndani yake kuna talanta saba. Rula hutusaidia kuweka mambo kwenye mstari. Penseli hutusaidia kuwa na malengo katika maisha. Pembetatu hutukumbusha haki na usawa kwa wote. Kipimapembe hutusaidia kujiheshimu na hutusaidia kupata maarifa. Kifutio hutukumbusha kuanza upya pale tunapokuwa tumekosea. Kichongeo hutusaidia kunoa penseli ili tuendelee kuwa na uwezo wa kujiwekea malengo katika maisha. Bikari hutukumbusha kuwa na mipaka katika maisha yetu. Angalia Shetani ameiba talanta gani katika mkebe wa maisha yako, na uirudishe talanta hiyo kwa gharama yoyote ile.

Bikari ikipotea utagombana na watu kila siku, hutakuwa na hekima ya kutenda jambo, kwani hutakuwa na mipaka katika kila jambo utakalolifanya. Kichongeo kikipotea hutafanikiwa katika maisha, kwa sababu hutakuwa na penseli ya kukuwezesha kuweka malengo katika maisha yako. Kifutio kikipotea, ukifanya kosa hutakuwa na uwezo wa kulisahihisha. Kipimapembe kikipotea hutapata maarifa na hutaheshimika.

Pembetatu ikipotea utaandamwa sana na watu wa haki za binadamu na watu wengine wote wanaopenda haki na usawa popote utakapokuwa. Penseli ikipotea hutakuwa na uwezo wa kujiwekea malengo katika maisha yako. Rula ikipotea ujue mambo yako hayatanyooka kamwe. Mkebe mzima ukipotea, hutakuwa na uwezo tena wa kuuona ufalme wa Mungu.

Hivyo, ni jukumu lako kuona ni talanta gani imechukuliwa na Shetani katika mkebe wa maisha yako na uirudishe kabla mlango wa rehema haujafungwa. Kwani mlango wa rehema ukifungwa, huku bado talanta zako hazijarudishwa, roho yako itaandikwa katika daftari la kuzimu na pengine usiokolewe kamwe.

No comments:

Post a Comment

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...