Friday 15 June 2018

Kufanikiwa Lazima Ushindikane

283. Kufanikiwa lazima ushindikane.

Kufanikiwa lazima umshinde Shetani. Wale waliofanikiwa kupitia nguvu za giza wamemshinda Shetani, kwa sababu Mungu ameruhusu wafanikiwe. Bila Mungu kuruhusu, hakuna atakayefanikiwa.

Wapo watu nomi waliobobea katika mambo ya giza lakini hawajafanikiwa; wamekwenda kwa wachawi na waganga wa jadi dunia nzima; na wapo watu wengi waliobobea katika mambo ya nuru lakini hawajafanikiwa; wamekwenda kwa wachungaji, mapadri na mashehe dunia nzima. Kwa nini? Kwa sababu Mungu hajaruhusu wafanikiwe. Lazima kuna sehemu wanakosea ndiyo maana Mungu hajawafungulia milango ya baraka.

Mungu anaweza kutumia mafanikio ya Shetani kwa faida ya watu wake. Mathalani, jambazi anaweza kujenga kanisa kwa ajili ya watu wa Mungu na Mungu akalibariki na akambariki jambazi, kwa sababu sifa kuu ya Mungu ni upendo. Jambazi anaweza kwenda kuiba akafanikiwa, wakati mchungaji anaweza kwenda kuhubiri akapata matatizo.

Mamafia wa Amerika ya Kusini na Kaskazini wanafanikiwa katika mambo yao, kwa sababu wanasaidia watu waliosahauliwa na serikali zao. Wanatoa upendo kwa Mungu, kwa kutoa upendo kwa wengine, ijapokuwa walifanikiwa kupitia nguvu za giza.

Katika giza lazima ushindikane, na katika nuru lazima ushindikane pia. Katika giza lazima ushindikane dhidi ya hila za Shetani, kwa kuwa mshirikina kwelikweli; na katika nuru lazima ushindikane dhidi ya hila za Shetani, kwa kuwa mlokole kwelikweli.

Kufanikiwa lazima ushindikane ama katika nuru au katika giza. Ukishindikana katika nuru umemshinda Shetani, ukishindikana katika giza umemshinda Shetani, lakini kwa ruhusa ya Mwenyezi Mungu.

Kubarikiwa, hata hivyo, si ishara ya kusamehewa dhambi. Kubarikiwa ni ishara ya kuwasaidia wengine.

No comments:

Post a Comment

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...