Friday 15 June 2018

Imani ya Wakristo Wengi Haina Macho

282. Imani ya Wakristo wengi haina macho. Wanaamini watu. Wanaamini kile watu wanachokisema, na kukiandika, badala ya kumwamini Mungu. Kumwamini mtu, au kuamini maandishi, badala ya kumwamini Mungu, ni sawa na kuabudu miungu wengine.

Weka akili yako pembeni kwa muda. Usiamini kile mtu anachokwambia, au usiamini kile unachokisoma kwenye vitabu. Lakini yachukue mawazo yao kisha yajaribishe katika mafundisho yako ya kiroho, ambayo tayari unayo, ili ujue kama kweli kile kilichosemwa au kuandikwa kinaleta maana katika maisha yako. Kama kinaleta, uko huru kumwamini Mungu. Lakini kama hakileti, ukimwamini Mungu umemwamini mungu mwingine.

Yesu na waandishi wote wa Biblia waliongea na kuandika kimafumbo, ili Neno la Mungu lijidhihirishe lenyewe kiroho katika mawazo ya mtu. Unaposikia Neno la Mungu kutoka kwa mtu acha lijidhihirishe lenyewe katika mawazo yako, kabla ya kumwamini au kutokumwamini Mungu.

No comments:

Post a Comment

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...