Shetani ukimwomba kitu, kama umesaini naye mkataba, anakupa hapohapo. Mungu ukimwomba kitu anaweza asikupe, kwani akikupa utakuwa muujiza ambao Mungu anaufanya kwa muda anaotaka yeye, na si muda anaotaka mwanadamu. Kwa hiyo huwezi kusema kwamba Mungu anaondoa uchawi wakati hujui kama ataondoa au hataondoa.
Bikira Maria alipomwomba Yesu afanye muujiza wa divai katika harusi huko Kana, Galilaya, Yesu alimshangaa na akasema saa yake ya kufanya muujiza ilikuwa bado haijawadia (Yohana 2:4). Mama na Mwana walikuwa na ushirika gani kati yao katika kutenda muujiza wa divai? Mama alitaka muujiza ufanyike hapohapo, lakini Mwana alikuwa na muda wake wa kuufanya muujiza huo.
Aidha, inaonekana kwamba ni mara chache sana kwamba wanaume hutolewa mapepo kwa kuomba msaada wa Mungu au sala za Watakatifu. Kwa hiyo inaonekana kwamba wanaweza tu kutolewa mapepo kwa msaada wa mapepo mengine, na ni kinyume cha sheria kutafuta msaada huo.
Mungu hakupi unachotaka. Anakupa unachostahili kupata. Wachungaji wangekuwa na uwezo wa kuondoa mapepo hapohapo, kila mgonjwa angekuwa anapona hapohapo.
Tatizo, hata hivyo, ni kwamba watu wengi hawajui kuomba! Ukiomba kitu ukapata kama ulivyoomba, kwa muda uliotaka, umepata kitu ambacho Roho wa Mungu alikuongoza kuomba. Kwa hiyo, usiache kumwambia Mungu akufundishe kuomba.
Wachungaji wanapaswa kuondoa mapepo kwa kidole cha Mungu na si kwa Beelzebuli, mkuu wa pepo.
No comments:
Post a Comment