Msitu
 wa Mvua wa Amazoni nchini Kolombia – na nchi zingine nane za kaskazini 
mwa bara la Amerika ya Kusini huko ‘Americas’ – magaidi wa Kolonia 
Santita walipokuwa wameficha tani 600 za madawa ya kulevya chini ya 
uangalizi wa waasi wa kisiasa wa Kolombia, Peru, Brazili, Venezuela na 
Bolivia, kabla ya kuzihamishia nchini Meksiko kwa ajili ya usambazaji wa
 dunia nzima. 
Ndani ya kitabu cha Kolonia Santita mtu mwenye historia kubwa na Msitu wa Amazoni ni Nicolas Kahima Kankiriho. Kankiriho alikuwa askari mamluki wa Uganda aliyetoroka na El Tigre katika nyambizi ya Jefe de Jefes SPD (‘the Silent Predator of the Deep’),
 iliyotengenezwa na Belinsky, katika Ghuba ya Meksiko Septemba 16, 1986.
 Msitu wa Amazoni ndiyo uliyomkuza Kankiriho, na ndiyo uliyompatia kazi 
kama mlinzi binafsi wa kiongozi wa Kolonia Santita. 
Msitu
 wa Amazoni ni msitu mkubwa kuliko misitu yote ya mvua ulimwenguni, 
wenye ukubwa wa kilometa za mraba milioni 5.5 (maili za mraba milioni 
2.123), uliotapakaa katika nchi tisa za Amerika ya kusini; ikiwemo 
Bolivia, Venezuela, Brazili, Peru, na Kolombia. 

No comments:
Post a Comment