Bunduki iliyotaka kumuua Mpelelezi wa Tume ya Dunia John Murphy 
Ambilikile huko Mexico City, MP5, iliyomuua Kiongozi wa CS-Copenhagen 
Regner Steiner Valkendorff huko San Antonio, Murphy alipokamatwa na 
Kolonia Santita baada ya kuiba kitabu cha siri katika makao makuu ya 
Kolonia Santita ya San Ángel. 
MP5 (‘Maschinenpistole 5’, au 
‘Machine Pistol Model 5’) ni mojawapo ya bunduki hatari zilizotengenezwa
 na Kiwanda cha Silaha cha Heckler & Koch GmbH cha Ujerumani; 
zilizotumiwa na makomandoo wa Tume ya 
Dunia na magaidi wa Kolonia Santita dhidi ya Kolonia Santita na dhidi ya
 Tume ya Dunia ya Kudhibiti Madawa ya Kulevya kwa mpangilio huo. MP5 ina
 uwezo wa kubeba kwa wakati mmoja risasi 100 katika chemba yake ya 
‘century’, kupiga risasi 900 kwa dakika (kwa kutumia mkanda wa risasi), 
na kufyatua risasi kwa kiasi cha kuleta maafa makubwa katika umbali wa 
meta 200 au futi 656. Mnamo mwaka 1980 katika Operation Nimrod ya Jeshi 
la Uingereza, MP5 ilijipatia umaarufu mkubwa duniani katika Ubalozi wa 
Irani huko Kensington jijini London; ilipotumiwa kwa mafanikio makubwa 
na makomandoo wa SAS, kuokoa mateka 26 dhidi ya magaidi 6 wenye msimamo 
mkali wa Irani, katika tukio lililoonyeshwa moja kwa moja na vituo vya 
televisheni.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
- 
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
 - 
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
 

No comments:
Post a Comment