Biblia
 pamoja na historia vinatwambia kuwa mitume kumi na wawili wa Yesu 
Kristo waliamua kufa kinyama kama mfalme wao alivyokufa, kwa sababu 
walikataa kukana imani yao juu ya Yesu Kristo. 
Mathayo
 alikufa kwa ajili ya Ukristo nchini Ethiopia kwa jeraha lililotokana na
 kisu kikali, Marko akavutwa na farasi katika mitaa ya Alexandria nchini
 Misri mpaka akafa, kwa sababu alikataa kukana jina la Yesu Kristo. 
Luka alinyongwa nchini Ugiriki kwa sababu ya kuhubiri Injili ya Yesu Kristo katika nchi ambapo watu hawakumtambua Yesu. 
Yohana
 alichemshwa katika pipa la mafuta ya moto katika kipindi cha mateso 
makubwa ya Wakristo nchini Roma, lakini kimiujiza akaponea chupuchupu, 
kabla ya kufungwa katika gereza la kisiwa cha Patmo (Ugiriki) ambapo 
ndipo alipoandika kitabu cha Ufunuo. Mtume Yohana baadaye aliachiwa huru
 na kurudi Uturuki, ambapo alimtumikia Bwana kama Askofu wa Edessa. 
Alikufa kwa uzee, akiwa mtume pekee aliyekufa kwa amani. 
Petro
 alisulubiwa kichwa chini miguu juu katika msalaba wa umbo la X 
kulingana na desturi za kikanisa za kipindi hicho, kwa sababu aliwaambia
 maadui zake ya kuwa alijisikia vibaya kufa kama alivyokufa mfalme wake 
Yesu Kristo. 
Yakobo
 ndugu yake na Yesu (Yakobo Mkubwa), kiongozi wa kanisa mjini 
Yerusalemu, alirushwa kutoka juu ya mnara wa kusini-mashariki mwa hekalu
 aliloliongoza la Hekalu Takatifu (zaidi ya futi mia moja kwenda chini) 
na baadaye kupigwa kwa virungu mpaka akafa, alipokataa kukana imani yake
 juu ya Yesu Kristo. 
Yakobo
 mwana wa Zebedayo (Yakobo Mdogo) alikuwa mvuvi kabla Yesu Kristo 
hajamwita kuwa mchungaji wa injili yake. Kama kiongozi wa kanisa 
hatimaye, Yakobo aliuwawa kwa kukatwa kichwa mjini Yerusalemu. Afisa wa 
Kirumi aliyemlinda Yakobo alishangaa sana jinsi Yakobo alivyolinda imani
 yake siku kesi yake iliposomwa. Baadaye afisa huyo alimsogelea Yakobo 
katika eneo la mauti. Nafsi yake ilipomsuta, alijitoa hatiani mbele ya 
hakimu kwa kumkubali Yesu Kristo kama kiongozi wa maisha yake; halafu 
akapiga magoti pembeni kwa Yakobo, ili na yeye akatwe kichwa kama mfuasi
 wa Yesu Kristo. 
Bartholomayo,
 ambaye pia alijulikana kama Nathanali, alikuwa mmisionari huko Asia. 
Alimshuhudia Yesu mfalme wa wafalme katika Uturuki ya leo. Bartholomayo 
aliteswa kwa sababu ya mahubiri yake huko Armenia, ambako inasemekana 
aliuwawa kwa kuchapwa bakora mbele ya halaiki ya watu iliyomdhihaki. 
Andrea
 alisulubiwa katika msalaba wa X huko Patras nchini Ugiriki. Baada ya 
kuchapwa bakora kinyama na walinzi saba, alifungwa mwili mzima kwenye 
msalaba ili ateseke zaidi. Wafuasi wake waliokuwepo katika eneo la tukio
 waliripoti ya kuwa, alipokuwa akipelekwa msalabani, Andrea aliusalimia 
msalaba huo kwa maneno yafuatayo: “Nimekuwa nikitamani sana na nimekuwa 
nikiitegemea sana saa hii ya furaha. Msalaba uliwekwa wakfu na Mwenyezi 
Mungu baada ya mwili wa Yesu Kristo kuning’inizwa juu yake.” Aliendelea 
kuwahubiria maadui zake kwa siku mbili zaidi, akiwa msalabani, mpaka 
akaishiwa na nguvu na kuaga dunia. 
Tomaso
 alichomwa mkuki nchini India katika mojawapo ya safari zake za 
kimisionari akiwa na lengo la kuanzisha kanisa la Yesu Kristo katika 
bara la India. 
Mathiya
 alichaguliwa na mitume kuchukua nafasi ya Yuda Iskarioti, baada ya kifo
 cha Yuda katika dimbwi la damu nchini India. Taarifa kuhusiana na 
maisha na kifo cha Mathiya zinachanganya na hazijulikani sawasawa. 
Lakini ipo imani kwamba Mathiya alipigwa mawe na Wayahudi huko 
Yerusalemu, kisha akauwawa kwa kukatwa kichwa. 
Yuda Tadei, ndugu yake na Yesu, aliuwawa kwa mishale alipokataa kukana imani yake juu ya Yesu Kristo. 
Mitume
 walikuwa na imani kubwa kwa sababu walishuhudia ufufuo wa Yesu Kristo, 
na miujiza mingine. Biblia ni kiwanda cha imani. Tunapaswa kuiamini 
Biblia kama mitume walivyomwamini Yesu Kristo, kwa sababu Biblia 
iliandikwa na mitume. 
Mitume
 kumi na wawili wa Yesu Kristo waliamua kufa kinyama kulinda heshima ya 
mfalme wao Yesu Kristo, kama Biblia na historia vinavyosema. Kwa nini 
watu (wengine) wa kizazi hiki wanasema hakuna Mungu na kwa sababu hiyo 
hawamwamini Yesu? Je, uko tayari kufa kwa ajili ya mtu aliyekufa kwa 
ajili yako? Kwa ajili ya mtu ambaye mitume walikuwa tayari kufa kwa 
ajili yake? Je, wewe una akili zaidi kuliko mitume? Yesu aliamua kufa 
ili wewe uishi, lakini bado unakuwa mbishi. Badilika. 

No comments:
Post a Comment