Bastola
 ya kalamu ya John Murphy Ambilikile aina ya Stinger; iliyotumiwa na 
Murphy kumuua kinyama jambazi sugu wa CS-Moscow – Tawi la Kolonia 
Santita nchini Urusi na nchi zote za Ulaya ya Mashariki; na baadhi ya 
nchi za Ulaya ya Kusini kama vile Masedonia, Montenegro, Uturuki na 
Ugiriki – Vladimir, huko Yugo Zapadnaya mjini Moscow, katika ‘dacha’ ya 
Kolonia Santita. 
Bastola
 ya kalamu aina ya Stinger (tamka ‘Sting’a’) ni silaha ‘halali’ kwa 
matumizi ya kawaida ya binadamu huko nchini Marekani hadi hii leo; 
halali kwa maana ya ATF – shirika la pombe, tumbaku na silaha la 
Marekani – kuichukulia kama silaha ya kawaida. Lakini Stinger ya John 
Murphy haikuwa (wala haijawahi kuwa) silaha ya kawaida! Ilitengenezwa 
kwa ajili ya matumizi ya Idara ya Usalama ya Tume ya Dunia (WIS – ‘WODEC
 Intelligence Services’) na kwa ajili ya matumizi ya Kikosi cha 
Kikomandoo cha Tume ya Dunia (EAC – ‘Executive Action Corps’). 
Stinger
 ya Murphy ilikuwa na uwezo wa kubeba risasi moja ndogo kwa wakati mmoja
 – iliyokuwa na ukubwa wa inchi 0.22 ya mtutu wa bunduki (‘.22 caliber’)
 – na kidonge kimoja cha ‘cyanide’ (‘potassium suicide pill’): ili 
akitekwa akimeze na kufa; kuliko kutoboa siri za EAC, na siri za Tume ya
 Dunia ya Kudhibiti Madawa ya Kulevya. 
Aidha,
 Stinger ya Murphy ilikuwa na uwezo wa kufyatua risasi ikiwa imenyooka 
(Stinger ya kawaida hufyatua risasi ikiwa imejikunja) na kifyatulio 
chake kilikuwa kwenye kichwa cha kalamu; na ilikuwa na koki mbili: moja 
kwa ajili ya risasi, na nyingine kwa ajili ya mrija wa kalamu, tofauti 
na Stinger ya kawaida ambayo ina koki moja, mbele ya kifyatulio. Stinger
 ya Murphy ilikuwa na uwezo wa kuandika kama kalamu ya kawaida! Ilikuwa 
na uwezo wa kutumia kiwambo cha kupunguza sauti, kama Stinger za 
kawaida. 


Kalamu ya John Murphy
ReplyDelete