Tuesday, 20 December 2016

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Guadalajara

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Guadalajara, Jalisco, Meksiko. Ndege ya Vijana wa Tume, Grumman Gulfstream IV, ilitua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Guadalajara saa saba usiku CST kutokea Copenhagen; Vijana wa Tume wakaingia Mexico City saa kumi alfajiri CST, katika mazingira ya kutatanisha.

Kamanda wa Jeshi la Polisi la Tume ya Dunia Kanda ya Amerika ya Kaskazini Meja Jenerali Sebastian Alejandro, na maafisa sita wa WODEC-Intelligence kutoka Mexico City, alikuwepo na wenzake katika Uwanja wa Ndege wa Guadalajara huko Jalisco kuwapokea Vijana wa Tume, kwa amri ya Jeshi la Anga la Meksiko ('Fuerza Aérea Mexicana') na Idara ya Usalama ya Tume ya Dunia, alipewa jukumu la kuwaingiza Vijana wa Tume jijini Mexico City kwa magari ya SUV na 'ambulance' kama wagonjwa mahututi. Katika nyumba yao ya siri waliyopewa na Jeshi la Anga la Meksiko, Calle Gante, Cuauhtémoc (tamka 'Kwauteimak'), katikati ya Mexico City, Vijana wa Tume walipata ugeni wa ghafla kama walivyoelezwa na Mkurugenzi wa Usalama wa Tume ya Dunia Christoffer Sortevik huko Copenhagen. Mmoja wa wageni hao (Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Meksiko (PGR) Virgilio Santo Graciano, Mkuu wa Jeshi la Polisi Meksiko (PJF) Demetrio Vega del Castilo, Kiongozi wa Kanda ya Amerika ya Kaskazini ya Tume ya Dunia Kamishna Profesa Randall Buchanan Ortega wa Marekani, Mkuu wa Mamlaka ya Kudhibiti Madawa ya Kulevya Marekani (DEA) Baxter Salvatore Sincere, na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Haki za Binadamu (CNDH) Daktari Santiago Luis-Fernando) alikuwa kibaraka wa Kolonia Santita, ingawa alikuwa kibaraka wa Kolonia Santita kwa shingo upande.

Wageni hao (viongozi wakubwa katika vita dhidi ya madawa ya kulevya duniani) walikwenda kuwajulia hali Vijana wa Tume na kuwapa hali halisi ya usalama ya Mexico City na ya Kateli ya Kolonia Santita; lakini miadi ya Vijana wa Tume na Debbie na Lisa (mtoto wa rais na mtoto wa naibu mwanasheria mkuu wa Meksiko kwa mpangilio huo) kesho yake katika Baa ya Desierto de Los Leones huko San Ángel, ilibadili kabisa historia ya Kolonia Santita na ya Tume ya Dunia.

No comments:

Post a Comment

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...