Friday, 9 December 2016
Siku ya Uhuru wa Tanzania
Tanganyika na Zanzibari ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 
Tanzania ikisambaratika Watanganyika watabaki na Tanganyika yao, na 
Wazanzibari watabaki na Zanzibari yao. Tarehe 26/4/1964 hatukupata 
uhuru. Tulishaupata tayari. Tuliungana Zanzibari na Tanganyika na 
kutengeneza Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibari, na miezi 
sita baadaye (tarehe 29/10/1964) nchi ikaitwa Jamhuri ya Muungano wa 
Tanzania. Makubaliano yakafanyika kuifanya tarehe 9/12/1961 kuwa tarehe,
 mwezi na mwaka rasmi wa uhuru wa taifa, na nchi zote zikataharifiwa, na
 kuanzia hapo kila tarehe 9/12 ya kila mwaka yakawa maadhimisho ya siku 
ya uhuru wa Tanzania kuanzia tarehe 9/12/1965. Hayati Mwalimu Julius 
Kambarage Nyerere akawa rasmi rais wa kwanza wa jamhuri hiyo, na Hayati 
Abeid Amani Karume akawa rasmi makamu wa kwanza wa rais wa jamhuri hiyo.
 Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Shehe Abeid Amani Karume walikuwa 
bendera ya taifa letu. Walikuwa alama ya amani, haki, uhuru, ujamaa, 
uzalendo, na Tanzania.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
- 
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
 - 
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
 

No comments:
Post a Comment