Friday, 9 December 2016
Siku ya Uhuru wa Tanzania
Tanganyika na Zanzibari ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Tanzania ikisambaratika Watanganyika watabaki na Tanganyika yao, na
Wazanzibari watabaki na Zanzibari yao. Tarehe 26/4/1964 hatukupata
uhuru. Tulishaupata tayari. Tuliungana Zanzibari na Tanganyika na
kutengeneza Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibari, na miezi
sita baadaye (tarehe 29/10/1964) nchi ikaitwa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania. Makubaliano yakafanyika kuifanya tarehe 9/12/1961 kuwa tarehe,
mwezi na mwaka rasmi wa uhuru wa taifa, na nchi zote zikataharifiwa, na
kuanzia hapo kila tarehe 9/12 ya kila mwaka yakawa maadhimisho ya siku
ya uhuru wa Tanzania kuanzia tarehe 9/12/1965. Hayati Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere akawa rasmi rais wa kwanza wa jamhuri hiyo, na Hayati
Abeid Amani Karume akawa rasmi makamu wa kwanza wa rais wa jamhuri hiyo.
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Shehe Abeid Amani Karume walikuwa
bendera ya taifa letu. Walikuwa alama ya amani, haki, uhuru, ujamaa,
uzalendo, na Tanzania.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...

-
Mercury Cougar ya John Murphy aliyonunua mwaka 1990 kwa gharama kubwa huko Michigan nchini Marekani. Gari hilo lililorekebishwa kwa ajili ...
-
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
-
Siku ya kuzaliwa ni siku ya kwanza ya safari nyingine ya siku 365, saa 5, dakika 48, sekunde 46 na maili milioni 600 kulizunguka jua. Safi...
No comments:
Post a Comment