Friday, 9 December 2016

Siku ya Uhuru wa Tanzania

Tanganyika na Zanzibari ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tanzania ikisambaratika Watanganyika watabaki na Tanganyika yao, na Wazanzibari watabaki na Zanzibari yao. Tarehe 26/4/1964 hatukupata uhuru. Tulishaupata tayari. Tuliungana Zanzibari na Tanganyika na kutengeneza Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibari, na miezi sita baadaye (tarehe 29/10/1964) nchi ikaitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Makubaliano yakafanyika kuifanya tarehe 9/12/1961 kuwa tarehe, mwezi na mwaka rasmi wa uhuru wa taifa, na nchi zote zikataharifiwa, na kuanzia hapo kila tarehe 9/12 ya kila mwaka yakawa maadhimisho ya siku ya uhuru wa Tanzania kuanzia tarehe 9/12/1965. Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akawa rasmi rais wa kwanza wa jamhuri hiyo, na Hayati Abeid Amani Karume akawa rasmi makamu wa kwanza wa rais wa jamhuri hiyo. Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Shehe Abeid Amani Karume walikuwa bendera ya taifa letu. Walikuwa alama ya amani, haki, uhuru, ujamaa, uzalendo, na Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...