Mimi ni mwana wa Mungu. Sisi sote ni watoto wa Mungu. Lengo la kuzaliwa
kwangu ni kufanya kazi pamoja na Roho Mtakatifu na malaika kumtumikia
Bwana, na kueneza injili ya Yesu Kristo duniani kote, kupitia vitabu.
Nilijifunza toka awali umuhimu wa kushindwa katika maisha ijapokuwa
nilijitahidi sana, na nilipoendelea kushindwa niliweka nadhiri ya
kufanya kitu kimoja kilicholeta maana zaidi katika maisha
yangu nacho ni uandishi wa vitabu. Uandishi wa vitabu ndicho kitu pekee
nilichokiweza zaidi kuliko vingine vyote na kuanzia hapo Mungu
aliniweka huru. Nilijua mimi ni nani. Nilijua kwa nini nilizaliwa.
Nilijifunza falsafa ya kuacha dunia katika hali nzuri kuliko
nilivyoikuta – kwa sababu hata mimi nilikuwepo – na falsafa ya kushindwa
si hiari. Maarifa hayo yakafanya niwe na heshima na upendo kwa watu
wote.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...

-
Mercury Cougar ya John Murphy aliyonunua mwaka 1990 kwa gharama kubwa huko Michigan nchini Marekani. Gari hilo lililorekebishwa kwa ajili ...
-
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
-
Siku ya kuzaliwa ni siku ya kwanza ya safari nyingine ya siku 365, saa 5, dakika 48, sekunde 46 na maili milioni 600 kulizunguka jua. Safi...
Kama si kwa ubatizo basi sisi ni watoto wa Mungu kwa uumbaji – kama inavyoonyeshwa katika vitabu vya Mwanzo, Wagalatia, Ezekieli, na Matendo ya Mitume.
ReplyDelete“Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.” (Mwanzo 1:26-27).
“Tazama, roho zote ni mali yangu; kama vile roho ya baba ni mali yangu, ndivyo ilivyo roho ya mwana mali yangu; roho ile itendayo dhambi itakufa.” (Ezekieli 18:4).
“Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Yesu Kristo. Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.” (Wagalatia 3:26-27).
“Kwa maana ndani yake yeye tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu. Kama vile mmoja wenu, mtunga mashairi alivyosema, , Maana sisi wote tu wazao wake.” (Matendo 17:28).
Yehova ‘humiliki’ kila mtu hapa duniani, na anaweza kutubariki au kutuadhibu kutegemeana na jinsi tunavyolipokea neno lake.