202.
 Matatizo ya kijamii, kimiiko, kimaadili, kisiasa, na kiroho; hayataweza
 kutatuliwa kwa pesa, vikao vya kifamilia, haki za binadamu, usalama wa 
taifa, au nguvu za kijeshi. Yataweza kutatuliwa kwa haki na hekima ya 
Mwenyezi Mungu. 
Israeli
 ilifikia kikomo cha kipindi chake kikubwa cha mafanikio tangu enzi za 
Sulemani. Taifa lilikuwa tajiri. Lilikuwa na nguvu. Lilikuwa na silaha 
nyingi na nzuri zaidi. Lilikuwa taifa lililojidai kwa uwezo wake mkubwa 
wa nguvu za kijeshi, hekima, ujasiri, utajiri, na faida za kimkakati. 
Nani angeweza kushindana na Israeli? Lakini Mungu hunguruma onyo kwamba 
uwezo wote mkubwa wa asili wa taifa, ujuzi waliojipatia, na sifa bora 
zaidi havikuweza kulisaidia taifa la Israeli. Watu huona nguvu ya taifa 
katika utajiri wake, idadi yake ya watu, silaha za kijeshi, teknolojia, 
na maarifa. Lakini Mungu huangalia haki. 
Kwa
 vile taifa la Israeli lilipoteza haki yake ya upendeleo, Mungu aliahidi
 kuliharibu kama alivyoyaharibu mataifa ya Waamori na Wamisri. Watu wa 
Israeli walishafika mbali sana kiasi cha Mungu kutokutegemea tena toba 
kutoka kwao. Kuna muda wa fursa na kuna muda ambao fursa haipo tena. 
Nafasi ya Israeli ya kutubu ilishafikia mwisho. 
Kama
 alivyokuwa amepigana vita vyao kwa ajili yao katika siku za nyuma sasa 
Mungu alipigana nao. Pamoja na ujasiri na utaalamu wao wote 
wasingependelewa tena. Mambo ambayo mwanzo yaliipa Israeli nguvu katika 
vita yaliwageukia. 
Israeli,
 kama adhabu kwa uozo wake wa kiroho na kimaadili, ilivamiwa na Ashuru 
katika mwaka wa 721 BC na kuangushwa vibaya katika vita hiyo kubwa. 
Waisraeli waliosalia walitekwa na kupelekwa uhamishoni ambako inaonekana
 walitoweka kabisa katika uso wa dunia hii. Hili lilikuwa ni jibu la 
Mungu kwa dhambi na uasi wao. 
Sababu
 ya kupanda na kuanguka kwa mataifa ni ya kimaadili na kiroho. Hakuna 
taifa linaloweza kutegemea nguvu na mali zake ili kujiokoa kutokana na 
madhara ya ukiukwaji wa maadili. 
Dhambi ikizidi katika taifa, Mungu ataliangamiza. Taifa likitenda haki, Mungu ataliinua. 

Uovu ni aibu kwa taifa zima!
ReplyDelete