Monday, 5 December 2016

Haki na Hekima ya Mwenyezi Mungu

202. Matatizo ya kijamii, kimiiko, kimaadili, kisiasa, na kiroho; hayataweza kutatuliwa kwa pesa, vikao vya kifamilia, haki za binadamu, usalama wa taifa, au nguvu za kijeshi. Yataweza kutatuliwa kwa haki na hekima ya Mwenyezi Mungu.

Israeli ilifikia kikomo cha kipindi chake kikubwa cha mafanikio tangu enzi za Sulemani. Taifa lilikuwa tajiri. Lilikuwa na nguvu. Lilikuwa na silaha nyingi na nzuri zaidi. Lilikuwa taifa lililojidai kwa uwezo wake mkubwa wa nguvu za kijeshi, hekima, ujasiri, utajiri, na faida za kimkakati. Nani angeweza kushindana na Israeli? Lakini Mungu hunguruma onyo kwamba uwezo wote mkubwa wa asili wa taifa, ujuzi waliojipatia, na sifa bora zaidi havikuweza kulisaidia taifa la Israeli. Watu huona nguvu ya taifa katika utajiri wake, idadi yake ya watu, silaha za kijeshi, teknolojia, na maarifa. Lakini Mungu huangalia haki.

Kwa vile taifa la Israeli lilipoteza haki yake ya upendeleo, Mungu aliahidi kuliharibu kama alivyoyaharibu mataifa ya Waamori na Wamisri. Watu wa Israeli walishafika mbali sana kiasi cha Mungu kutokutegemea tena toba kutoka kwao. Kuna muda wa fursa na kuna muda ambao fursa haipo tena. Nafasi ya Israeli ya kutubu ilishafikia mwisho.

Kama alivyokuwa amepigana vita vyao kwa ajili yao katika siku za nyuma sasa Mungu alipigana nao. Pamoja na ujasiri na utaalamu wao wote wasingependelewa tena. Mambo ambayo mwanzo yaliipa Israeli nguvu katika vita yaliwageukia.

Israeli, kama adhabu kwa uozo wake wa kiroho na kimaadili, ilivamiwa na Ashuru katika mwaka wa 721 BC na kuangushwa vibaya katika vita hiyo kubwa. Waisraeli waliosalia walitekwa na kupelekwa uhamishoni ambako inaonekana walitoweka kabisa katika uso wa dunia hii. Hili lilikuwa ni jibu la Mungu kwa dhambi na uasi wao.

Sababu ya kupanda na kuanguka kwa mataifa ni ya kimaadili na kiroho. Hakuna taifa linaloweza kutegemea nguvu na mali zake ili kujiokoa kutokana na madhara ya ukiukwaji wa maadili.

Dhambi ikizidi katika taifa, Mungu ataliangamiza. Taifa likitenda haki, Mungu ataliinua.

1 comment:

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...