201. Shetani lengo lake ni kutawala dunia. Huwezi kutawala dunia bila elimu!
Shetani anajua kwamba sisi ni warithi wa wokovu na kwamba dunia hii
ni kitu kilichoahidiwa kwa Ibrahimu na watoto wake. Sisi wote ni watoto
wa Ibrahimu. Anajua kabisa kwamba baadaye sisi ndiyo tutakaokuwa
watawala halisi wa dunia hii. Hivyo, anajitahidi kwa kadiri ya uwezo
wake wote ili hilo lisitokee. Shetani na malaika wake ni wengi sana, na
wanatumia kila silaha waliyokuwa nayo kutawala dunia.
Inavyoonekana,
kadiri mtu anavyozidi kupata elimu ndivyo anavyozidi kudharau uwepo wa
Shetani na uwepo wa Mungu pia. Lakini, kwa upande mwingine, ndivyo
anavyoonekana hajasoma sana na ndivyo Shetani anavyozidi kulaumiwa kwa
kila dhambi inayotendeka. Kuna elimu ya kidunia na kuna elimu ya kidini.
Huwezi kutawala dunia bila elimu ya kidunia, kwa sababu Shetani anajua
ukiipata elimu hiyo hutajua kama yupo; na huwezi kutawala dunia bila
elimu ya kidini, kwa sababu Mungu anajua ukiipata elimu hiyo utajua kama
yupo. Hivyo, utamdharau Mungu ukipata elimu ya kidunia, utamheshimu
Mungu ukipata elimu ya kidini.
Kama Shetani anatumia elimu
kutawala dunia kama vile Mungu anavyotumia elimu kutawala dunia, nani
alisema kuwa baadhi ya wasanii wa ‘Bongo Movie’ na ‘Bongo Flava’ ni
wanachama wa chama cha siri cha kusaidiana cha wajenzi huru? Je, wana
elimu? Jibu unalo.
Anayesema fulani ni mwanachama wa chama cha
siri cha kusaidiana cha wajenzi huru ana hakika? Haya mambo ni siri.
Amejuaje? Kumbuka, usiamini, jua.
Kama wana elimu wanaweza kuwa wajenzi huru; lakini kama hawana elimu, hawawezi kuwa wajenzi huru.
Shetani
ni mjanja sana. Anajua bila elimu hataweza kutawala dunia, baada ya
mpango wa Mungu kukamilika. Anajua, mtu akipata elimu ni rahisi sana
kujua kama Shetani hayupo. Hivyo Shetani atatimiza malengo yake bila
watu kujua.
Mungu hatakubali kuwa na mtu katika ufalme wake ambaye
hatakubali kutawaliwa naye. Usikubali kutawaliwa na Ibilisi, kubali
kutawaliwa na Mungu. Ni jukumu letu kuanza kuishi sasa kama vile
tutakavyoishi mbinguni. Shetani anataka uwe na hekima ya duniani ili
akupumbaze. Lakini hofu ya Mungu ndiyo msingi wa hekima ya kweli.
Ukitaka asikupumbaze, pokea roho ya Mungu kwa kubatizwa. Ukiipokea roho
ya Mungu utajua mambo ya Mungu, ambayo dunia haiwezi kujua.
http://www.facebook.com/koloniasantita
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...

-
Mercury Cougar ya John Murphy aliyonunua mwaka 1990 kwa gharama kubwa huko Michigan nchini Marekani. Gari hilo lililorekebishwa kwa ajili ...
-
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
-
Siku ya kuzaliwa ni siku ya kwanza ya safari nyingine ya siku 365, saa 5, dakika 48, sekunde 46 na maili milioni 600 kulizunguka jua. Safi...
Usipoangalia kwa undani sana, Shetani anatutawala kwa sababu hatuna uwezo wa kumwona. Aidha, anaweza, bila hata sisi kujua, kuwasiliana nasi kimawazo na kitabia kupitia hewa hiihii inayotusaidia katika kuishi. Wengi katika dunia hii hawajui kama wanadanganywa au walishadanganywa tayari. Shetani hataki tujue kama anatudanganya au ameshatudanganya tayari, na hataki tujue kama yuko hapa kwa ajili ya kutudanganya sisi. Tunajua tu kwa sababu Neno la Mungu hudhihirisha ukweli huu kupitia Roho Mtakatifu na malaika wema, na tunauamini. Licha ya hili jambo kutokea katika maisha yetu, Shetani bado anaweza kutudanganya hadi pale tutakapoerevuka kwa kiasi cha kutosha kuhakikisha kwamba udanganyifu huo hautatokea tena.
ReplyDelete