198. Huna mama huna mtetezi. Jitetee!
Mama anaweza kufa ili mwanawe aishi, anaweza kufunga na kuomba ili
mwanawe Mungu amsaidie ashinde mtihani wake, anaweza kulala njaa ili
mwanawe ale, anaweza kujitolea vitu vingi au mambo mengi katika maisha
yake ili mwanawe aishi vizuri, anaweza kuingia dhambini ili mwanawe
asamehewe.
Kama huna mama, kama mama yako alishafariki, au kama yupo lakini
hakujali, hata kama baba yako yupo au hayupo, mafanikio yako yatatokana
na juhudi zako mwenyewe.
Isipite siku
hata moja katika maisha yako bila kusema hata kimoyomoyo kwa wazazi wako
na kwa watu wote wanaokupenda kwamba unawapenda, kwani siku moja
hawatakuwepo tena.
http://www.facebook.com/koloniasantita
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
-
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
-
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
-
Uwanja wa Ndege wa Copenhagen-Roskilde: uliotumiwa na Tume ya Dunia na Kolonia Santita kwa pamoja – kilometa tisa kutoka katika Kanisa ...

Hata wahenga walisema, “Mtegemea cha nduguye hufa maskini.”
ReplyDeleteMama anaweza kuingia dhambini ili mwanawe asamehewe (kwa mfano anaweza kwenda kwa mganga wa kienyeji kwa ajili ya mafanikio ya mwanawe, na kadhalika).
ReplyDelete