199. Utajiri una changamoto nyingi. Yesu alisema ni rahisi kwa ngamia
kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa
Mungu. Hakusema msomi. Usiwe mwendanguu. Jikusuru kuujua ukweli.
Usiwe mwendanguu (usiwe mtu aliyekata tamaa kabisa). Jikusuru (jitahidi kwa kadiri ya uwezo wako wote) kuujua ukweli.
Lakini
ukweli ni upi? Ukweli ni kwamba utajiri una changamoto nyingi kuupata
na kuudumisha pia kuliko usomi na kwamba ukweli ni amani ya Mungu katika
moyo wa mwanadamu. Heri msomi kuliko tajiri – Heri yule aliyesoma
kuliko tajiri asiyesoma au yule aliyesoma kuliko vile alivyosoma tajiri
au tajiri asiyesoma au aliyesoma lakini asiyekuwa na tamaa kabisa na
dunia hii ambaye kukosa kwake tamaa na dunia hii kunamfanya msomi.
Ndivyo Kristo anavyomaanisha. Si kwamba tajiri hawezi kuuona ufalme wa
mbinguni. Ibrahimu, Isaka, Yakobo, Yusufu, Daudi, Sulemani, Yehoshafati,
Hezekia, Zakayo, Yoana, Susana, na Lidia watauona ufalme wa mbinguni na
walikuwa matajiri. Mali zao zilivyozidi hawakuangalia moyoni, hawakuwa
na tamaa kabisa na dunia hii, bali walimtumaini Mungu kwa kila kitu
walichokuwa nacho. Anaweza. Lakini asiipende dunia bali ayapende mambo
ya ufalme wa Mungu kwa moyo wake wote.
http://www.facebook.com/koloniasantita
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...

-
Mercury Cougar ya John Murphy aliyonunua mwaka 1990 kwa gharama kubwa huko Michigan nchini Marekani. Gari hilo lililorekebishwa kwa ajili ...
-
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
-
Siku ya kuzaliwa ni siku ya kwanza ya safari nyingine ya siku 365, saa 5, dakika 48, sekunde 46 na maili milioni 600 kulizunguka jua. Safi...
Yoana mkewe Kuza (wakili wake Herode) pamoja na Susana walihubiri injili na walitoa mchango mkubwa katika mazishi ya Yesu Kristo pamoja na Mariamu Magdalene; Yusufu ‘Mwana wa Faraja’ aliuza shamba lake na kupeleka fedha miguuni pa mitume kwa ajili ya injili; na Lidia alianzisha kanisa la kwanza katika bara la Ulaya nyumbani kwake.
ReplyDeleteHata kama umetajirika kiasi gani mpe Mungu kipaumbele cha kwanza katika kila jambo unalofanya. Toa zaka na sadaka na jitolee katika mambo yote yanayompendeza Mungu.
ReplyDeleteMungu anataka tuwe na mtazamo wa ‘kila kitu kinawezekana juu ya jua’ na si ‘kila kitu kinawezekana chini ya jua’.
ReplyDeleteTajiri asiyesoma lakini anayejali mambo ya ufalme wa Mungu kuliko anavyoijali dunia au yule aliyesoma lakini anayejali mambo ya ufalme wa Mungu kuliko anavyoijali dunia ni msomi. Anaweza kuuona ufalme wa Mungu.
ReplyDelete