Chumba cha John Murphy katika Hoteli ya Sophie Amalie jijini
Copenhagen, iliyoko katika mtaa uitwao Sankt Annæ Plads, John Murphy
alipofikia badala ya Hoteli ya Astoria ambapo magaidi wa Kolonia Santita
wangemmaliza.
Sophie Amalie Hotel ni hoteli ya kisasa ya
kimataifa yenye hadhi ya nyota nne daraja la kwanza iliyoko jirani na
Kasri la Kifalme la Amalienborg, kumbukumbu ya malkia wa karne ya kumi
na saba wa Denmaki Malkia Sophie Amalie. Murphy alikaa Sophie Amalie
Hotel chumba namba 117 kwa dakika 45 – kabla ya kutuma watu baadaye
kwenda kuchukua mizigo yake na kuipeleka Makao Makuu ya Tume ya Dunia
Vesterbrogade – kabla ya kuhamia Hellerup (kaskazini ya Copenhagen
Mjini, au ‘Indre By’) katika nyumba ya siri ya mpelelezi wa Tume ya
Dunia Frederik Mogens kutoka Denmaki.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
-
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
-
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
-
Uwanja wa Ndege wa Copenhagen-Roskilde: uliotumiwa na Tume ya Dunia na Kolonia Santita kwa pamoja – kilometa tisa kutoka katika Kanisa ...

No comments:
Post a Comment