Mimi, Profesa Ken Walibora na Profesa Mukoma wa Ngugi (mtoto wa Profesa
Ngugi wa Thiong’o wa Kenya) baada ya mimi na Mukoma kuhojiwa na Ken
kuhusiana na Tuzo ya Kiswahili ya Mabati-Cornell ya Fasihi ya Kiafrika,
katika Hoteli ya Serena Nairobi. Mukoma wa Ngugi ni profesa wa
Kiingereza katika Chuo Kikuu cha Cornell cha New York nchini Marekani.
Yeye na Dkt Lizzy Attree (mkurugenzi wa tuzo ya juu zaidi kati ya tuzo
zote za uandishi wa vitabu barani Afrika ya Caine) ndiyo waanzilishi wa
Tuzo ya Kiswahili ya Mabati-Cornell ya Fasihi ya Kiafrika iliyoanzishwa
huko Nijeria mwaka 2014.
http://www.enockmaregesi.wordpress.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...

-
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
-
Uwanja wa Ndege wa Copenhagen-Roskilde: uliotumiwa na Tume ya Dunia na Kolonia Santita kwa pamoja – kilometa tisa kutoka katika Kanisa ...
No comments:
Post a Comment