Bustani za Tivoli, katikati ya kituo kikubwa cha treni cha Hovedbanegård
na kituo kikubwa cha mabasi cha Rådhuspladsen, ni bustani kubwa za
michezo na mapumziko za Copenhagen. Bustani hizi ndizo zilizotumika
kuwapoteza majambazi wa Kolonia Santita katika harakati za kumwokoa
Daniel Yehuda wa bandia, katika Machafuko ya Sheraton jijini Copenhagen.
http://www.enockmaregesi.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
-
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
-
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
-
Uwanja wa Ndege wa Copenhagen-Roskilde: uliotumiwa na Tume ya Dunia na Kolonia Santita kwa pamoja – kilometa tisa kutoka katika Kanisa ...

Majambazi wa Kolonia Santita Regner Steiner ('Kimbunga') na Ulla Wagner ('Death Queen'); walivyokimbia wakiwa ndani ya magari mawili ya kihuni, Polisi wa Tume na wa Copenhagen waliwaona vizuri. Polisi waliingia katika magari yao kwa pupa na kuwafukuza maadui kwa nguvu zao zote, lakini maadui wakawashinda nguvu. Maadui walionekana kuwa mafundi stadi wa kuendesha magari, bila hata kujali watu na magari mengine mabarabarani. Kimbunga alijizungusha nje ya Bustani za Tivoli kwa muda mrefu na hatimaye kujikuta akiwauza kabisa polisi wa tume na polisi wa Copenhagen; lakini Ulla, aliyekimbilia upande mwingine wa Barabara ya Søgade, hakufika mbali hata hivyo. Alizingirwa, ghafla, na magari mengine ya polisi ambayo kwa kipindi kile yalikuwa yakitokea katika kituo kikuu cha polisi cha Tume ya Dunia kilichopo Århusgade.
ReplyDelete