Monday 8 July 2013

Amani

40. Kuikaribisha amani ya Mungu katika maisha yangu kumenisaidia. Naishi mbinguni duniani.

Huu ndiyo mwisho wa sehemu ya kwanza ya Falsafa za Kolonia Santita. Kuanzia Jumatatu ijayo – kila Jumatatu bila kukosa kwa miezi sita mfululizo – nitakuwa naweka misemo, mmojammoja, hapa Blogger na Wordpress itakayoitwa Falsafa za Enock Maregesi. Usikose Kitendawili cha Kolonia Santita leo saa 8:00 mchana kwa saa za Afrika Mashariki. Huu ni msemo wa arobaini katika tovuti za Blogger, Wordpress na Facebook; na wa sabini katika tovuti ya Goodreads. Falsafa za Kolonia Santita (sehemu ya kwanza na ya pili) zitaendelea mpaka kufikia mia moja na hamsini.

www.facebook.com/koloniasantita

5 comments:

  1. Zawadi bora ya maisha kwa mwanadamu si fursa ya kufanya kazi kwa bidii na kuwa kitu fulani katika jamii. Ni amani ya Mungu katika moyo wa mwanadamu.

    ReplyDelete
  2. Amani ni paradiso ya duniani.

    ReplyDelete
  3. Amani ya Mungu lazima itawale hapa duniani, la sivyo.....

    ReplyDelete
  4. Hongera kwa kumaliza sehemu ya kwanza ya Falsafa za Kolonia Santita,ni matumaini yangu hata falsafa za Enock Maregesi zitamalizika vizuri. God bless.

    ReplyDelete

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...