Friday 15 June 2018

Kibiritingoma

287. Umewahi kutongoza mwanamke akajishauri kukukubali badala ya kujishauri kukukataa? Umewahi kutongoza mwanamume akajishauri kukukataa badala ya kujishauri kukukubali? Ndugu yangu, yashinde majaribu.

Sababu kubwa inayofanya mwanamke au mwanamume ajishauri kumkubali mwanamume au mwanamke badala ya kujishauri kumkataa ni nguvu ya uchumi aliyonayo mwanamume au mwanamke anayetongoza. Kumkataa mtu mwenye nguvu ya uchumi ni vigumu sana hata awe mbaya kiasi gani. Maana nguvu ya uchumi haiangalii sura wala umbile la mtu.

Mwanamke anayejishauri kumkubali mwanamume yeyote mzuri au mwenye pesa, au mbaya na mwenye pesa, au mzuri na mwenye pesa, ni kibiritingoma. Yule anayejishauri kukataa ni muungwana.

Mwanamume anayejishauri kumkataa mwanamke yeyote mzuri au mwenye pesa, au mbaya na mwenye pesa, au mzuri na mwenye pesa, ni muungwana. Yule anayejishauri kukubali ni kibiritingoma.

Kuna tamaa ya ngono na kuna tamaa ya pesa. Mwanamume ana tamaa ya ngono na mwanamke ana tamaa ya pesa, na kinyume chake.

Yashinde majaribu yako, kwani nguvu kubwa ya Shetani imejificha katika mafanikio.

Mwanamume kumtongoza mwanamke au mwanamke kumtongoza mwanamume akakubali au akakataa kirahisi, au vinginevyo, ni jaribu ambalo kila mtu anapaswa kulishinda kwa hekima ya Mungu.

Kiungo cha binadamu kinachofanya watu waongezeke hatukupewa ili tukitumie kwa anasa za ulimwengu huu. Tulipewa kwa ajili ya kuongezeka tukiwa katika taasisi rasmi ya ndoa, kama upendo wa Yesu Kristo na Kanisa, na kwa ajili ya starehe ya macho kama ilivyorekodiwa katika kitabu cha mapenzi cha Biblia kiitwacho Wimbo Ulio Bora.

Mungu alipomuumba Adamu na Hawa amri ya kwanza aliyowapa ni kufanya mapenzi, ili waijaze dunia, wakiwa katika taasisi ya ndoa. Hivyo, mapenzi nje ya taasisi ya ndoa ni dhambi inayostahili aibu.

No comments:

Post a Comment

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...