277. Watanzania wengi wanafanya makusudi angalau wapate chochote.
Usifanye makosa kwa makusudi kuvifurahisha vizazi vya leo na kulishibisha tumbo lako na matumbo ya familia yako. Ukifanya hivyo, vizazi vya leo na vya kesho vyenye akili vitakucheka.
Kwani ukifanya kosa kwa makusudi wapo watu watakaogundua kuwa umefanya kosa, na hao watu watakudharau, iwapo watagundua kuwa umefanya kosa kwa makusudi, hata kama hiyo dharau hawatakuonyesha hadharani. Lakini, hilo kosa, baadaye, litafanya udharaulike waziwazi wewe na familia yako.
Hata kama watu hawaonekani kuziona juhudi zako, fanya kazi kwa bidii na maarifa, kwani, kwa taarifa yako, wanaziona.
No comments:
Post a Comment