271. Ukishakuwa mtawala wa kitaifa umeua! Ama kwa kujua au kutokujua! Ama kwa kupenda au kutokupenda!
Taifa ni malaika! Taifa ni Shetani! Laana ya mwenye haki ina haki.
Taifa kama lina haki, mwananchi kama ana haki, laana yake ina haki. Lakini kama taifa halina haki, mwananchi hana haki, vilevile laana yake haitakuwa na haki.
Mtawala wa kitaifa anaweza kufanya maamuzi mazito yanayoweza kuleta madhara makubwa anayoyajua au asiyoyajua.
Wananchi (na watawala) wanapaswa kutumia busara na hekima kuyakubali au kuyakataa maamuzi ya viongozi wao, na wawe na hofu ya Mungu, yawe mema au mabaya.
Vilevile, kila mtu, mtawala au mwananchi wa kawaida, anapaswa kuwa na busara na hekima juu ya maamuzi yake. Maamuzi yoyote yale yanaweza kuwa na madhara makubwa kwa mwananchi au taifa.
Monday 2 April 2018
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
-
Mercury Cougar ya John Murphy aliyonunua mwaka 1990 kwa gharama kubwa huko Michigan nchini Marekani. Gari hilo lililorekebishwa kwa ajili ...
-
Siku ya kuzaliwa ni siku ya kwanza ya safari nyingine ya siku 365, saa 5, dakika 48, sekunde 46 na maili milioni 600 kulizunguka jua. Safi...
-
41. Ukitaka kuwa mfanyabiashara mzuri wa madawa ya kulevya usitumie madawa ya kulevya. Siri ya mafanikio ya Kolonia Santita ni nidhamu na ...
No comments:
Post a Comment