Mbegu tunazopanda leo ni mazao ya msimu ujao. Ukipanda mbegu mbaya
utavuna mabaya. Ukipanda mbegu nzuri utavuna mazuri. Ukitenda mabaya leo
kesho yako itakuwa mbaya. Ukitenda mazuri leo kesho yako itakuwa nzuri.
Okoa kesho leo kwa kupanda mbegu nzuri na kuzimwagilia kwa
imani na upendo kwa watu. Mungu ataleta mvua, jua na ustawi wa mazao
yako.
Panda mbegu ya msamaha kwa maadui zako, uvumilivu kwa
wapinzani wako, tabasamu kwa marafiki zako, mfano bora kwa watoto wako,
uchapakazi kwa kazi zako, uadilifu kwa waajiri wako na kwa wafanyakazi
wako pia kama unao, ndoto kwa malengo yako, na uaminifu kwa marafiki
zako wa ukweli. Kila mbegu irutubishwe kwa mapenzi huru yasiyokuwa na
masharti yoyote, au mapenzi huru yasiyokuwa na unafiki wa aina yoyote
ile.
Usifiche vipaji vyako. Ukiwa kimya utasahaulika. Usipopiga hatua utarudi nyuma. Usiwe na hasira, wivu au ubinafsi.
Fanya kazi kwa bidii leo kuokoa kesho yako kesho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...
-
KITENDAWILI CHA KOLONIA SANTITA Shilingi milioni moja za Kitanzania kushindaniwa ndani ya miezi sita kuanzia leo Swali: Kila namba ...
-
Mpelelezi wa Tume ya Dunia kutoka Jerusalem, Israeli, Kanali Daniel ‘Yehuda Ben-Asher’ Ebenezer, Daniel Yehuda, alikuwa komandoo wa kit...
-
Uwanja wa Ndege wa Copenhagen-Roskilde: uliotumiwa na Tume ya Dunia na Kolonia Santita kwa pamoja – kilometa tisa kutoka katika Kanisa ...

No comments:
Post a Comment