Sunday, 9 October 2016

Hiroglifu ya Kolonia Santita

Hiroglifu ya Kolonia Santita ni alama inayotumiwa na vituo vya udhibiti wa magonjwa (CDC) na taasisi za afya za kitaifa (NIH) duniani kote. Hutumiwa na Kolonia Santita kwa sababu Panthera Tigrisi au El Tigre (jambazi mkuu wa Kolonia Santita na mfalme wa madawa ya kulevya duniani) anamiliki makampuni ya kikemia na ujenzi katika mabara yote ya Amerika na katika bara la Asia. Rangi nyeusi inawakilisha nguvu za giza, rangi nyekundu inawakilisha hatari, vichwa vitatu vya sururu vinawakilisha biashara, na chembe tatu za bunduki zinawakilisha halafa. Katika hiroglifu (hieroglifu) vichwa vitatu vya sururu na chembe tatu za bunduki za Kalashnikov; na alama ya bahati, mafanikio, udhalimu na mwanzo mpya ya msalaba wa swastika, hutumika kama alama ya ujenzi na halafa ya Kolonia Santita. Alama hii inatumika hata katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, na inatambuliwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

1 comment:

  1. Kolonia Santita ni shirika la madawa ya kulevya la Meksiko na Kolombia. Lina wanachama hai zaidi ya 450,000 duniani kote.

    ReplyDelete

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...