Monday, 18 July 2016

Julai 29

182. Je, ni kweli kwamba dunia itaisha mwezi huu tarehe 29? Hakuna ajuae, tujiandae.

http://www.mirror.co.uk/news/weird-news/world-end-july-29-according-8411169

3 comments:

  1. Wanasayansi wanaamini kuwa Yesu atarudi tarehe 29 Julai 2016. Tarehe hiyo kitu kikubwa sana kitatokea katika dunia yetu kitakachosababisha tetemeko kubwa la ardhi, litakalosababishwa na kubadilika kwa ncha za dunia, tendo litakalosababisha mionzi ya gama kutoka kwenye jua ifike duniani na kuua kila kitu kinachoonekana katika uso wa dunia hii. Watakatifu watafufuka na kumlaki Kristo mawinguni, ambaye anakuja kuwachukua wateule na kumweka Shetani kifungoni kwa miaka 1000. Hayo yote, wanasema, yatatokea ndani ya siku 11 kuanzia leo. Yaani, kusini mwa dunia kutakuwa kaskazini mwa dunia, kaskazini mwa dunia kutakuwa kusini mwa dunia.

    Kitendo hicho kitafanya dunia ikose kinga ya sumaku iitwayo ‘magnetosphere’ ambayo hukinga dunia dhidi ya mionzi ya gama kutoka kwenye jua. Mionzi hiyo hugonga ukuta wa ‘magnetosphere’ kila baada ya dakika 8 kwa mwendokasi wa kilometa milioni 1080 kwa saa; na kusambazwa katika ncha za dunia ambapo aghalabu huchanganyikana na oksijeni na kutengeneza kitu kinaitwa ‘aurora’, au mwanga wa ncha, ambacho ni maajabu mengine ya angani. Mwaka 2012 wanasayansi walisema ncha za dunia zingebadilika lakini hazikubadilika. Je, muda umefika sasa wa kuwaamini wanasayansi? Biblia ni chuo cha Mungu. Soma Biblia kupata maarifa.

    Ukiwa karibu na Mungu utakuwa na maarifa kuliko profesa, Mungu ana maarifa kuliko profesa.

    ReplyDelete
  2. Hakuna ajuae siku wala saa.

    ReplyDelete
  3. Nukuu ya ‘Julai 29’ inakutaka wewe, mimi na wengine wote kuwa tayari kwa ajili ya ujio wa Yesu Kristo. Si kuwa tayari kwa ajili ya Julai 29. Kamwe mwanasayansi, au binadamu mwingine yoyote yule, hatajua Mungu anafikiria nini.

    ReplyDelete

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...