181. Damu, mto wa maisha unaotiririsha maji yake mwilini kwa kusukumwa
na pampu za moyo na kuchujwa na fizi za mapafu, inaundwa na seli na maji
yaitwayo utegili au maji ya damu, ambayo kazi yake ni kusafirisha
oksijeni na virutubisho katika kila sehemu ya mwili, ndani yake kuna
roho. Mungu alitoa kafara ya damu kwa ajili ya Adamu na Hawa katika
Bustani ya Edeni. Ibrahimu alitoa kafara ya damu kwa ajili ya Israeli
ijapokuwa mapenzi ya Mungu kwa Israeli yalikwisha baada ya kusulubiwa
kwa Yesu Kristo. Wana wa Israeli walitoa kafara za damu kwa ajili ya
wokovu wa watoto wao wa kwanza na watoto wa kwanza wa wanyama wao nchini
Misri. Mungu alitoa kafara ya damu ya Yesu Kristo nchini Israeli kwa
ajili ya wanadamu wote duniani. Damu ya mwanakondoo ina nguvu kuliko
maombi, imetiwa wakfu na Mwenyezi Mungu na ina uhusiano mkubwa na
ulimwengu wa roho. Ukifunikwa na damu ya mwanakondoo Shetani hatakuona.
Shetani asipokuona, utafanikiwa.
http://www.facebook.com/koloniasantita
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Roho Yako
289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...

-
Mercury Cougar ya John Murphy aliyonunua mwaka 1990 kwa gharama kubwa huko Michigan nchini Marekani. Gari hilo lililorekebishwa kwa ajili ...
-
120. Wakati mwingine tukitaka kutambulika hatuna budi kuweka mbele aibu ya heshima yetu. http://www.enockmaregesi.wordpress.com
-
179. Yesu alipokuwa msalabani watu wengi walimzunguka. Askari wa Kirumi aliyekuwa na chongo, na mkuki, alikuwa na jukumu la kumtesa Yesu ...
Siku ya kwanza dhambi ya kwanza ilipotendwa Mungu alitoa kafara ya kwanza ya mnyama kwa ajili ya wazazi wetu wa kwanza Adamu na Hawa. Adamu na Hawa walikuwa uchi, baada ya kutenda dhambi, Mungu akawalaani lakini akawapa uwezo wa muda mfupi wa kutubu dhambi zao ili awasamehe! Kutokana na ngozi za wanyama hao walipata mavazi na kutokana na damu ya wanyama hao walipata fursa ya kuishi na kutubu dhambi zote walizozitenda. Bila hivyo wasingepata muda wa kusamehewa.
ReplyDeleteKama damu haina maana kwa nini Mungu anaipenda? Kama damu haina maana kwa nini Shetani anaipenda? Mungu ni roho, Shetani ni roho, lakini damu ni kitu kinachoonekana kwa macho. Kwa nini damu ni kitu cha muhimu kiasi hicho kwa Mungu na kwa Shetani pia? Damu ni pato la ziada la ufunuo wa kiroho. Yaani, damu ni sehemu ya ulimwengu wa roho. Mungu ndiye aliyetengeneza damu kwa malengo anayoyajua yeye mwenyewe, hata Shetani hajui kwa asilimia mia umuhimu wa damu katika ulimwengu unaoonekana na katika ulimwengu usioonekana. Damu ina uwezo wa kuzuia mapepo kutoka kuzimu yasiharibu mipango ya maisha ya watu na ina uwezo wa kuondoa dhambi. Kafara ya damu inapotolewa inaimarisha uhusiano kati ya mtu na ulimwengu wa roho. Roho unayoitolea kafara inasikiliza shida zako papo hapo na kila unachoomba aghlabu kinatekelezwa. Ukitoa kafara kwa ajili ya Shetani, Shetani atasikiliza shida zako. Ukitoa kafara kwa ajili ya Mungu, Mungu atasikiliza shida zako. Tatizo kubwa la mwanadamu ni dhambi! Jibu la tatizo hilo ni damu ya Yesu Kristo. Imani ya mwanakondoo ni imani ya kweli! Imani ya mwanambuzi ni imani ya mashaka.