Siku
ya Alhamisi tarehe 3 Desemba 2015 nilipokea rasmi tuzo yangu ya
Mabati-Cornell ya Fasihi ya Kiafrika jijini Nairobi nikiwa na washindi
wenzangu Anna Samwel Manyanza, Mohammed Khelef Ghassani na Christopher
Bundala Budebah. Hiki ni kitu kikubwa sana kutokea katika maisha yangu ya uandishi wa vitabu.
Awali
ya yote ningependa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunifikisha siku hiyo
na kunidhihirishia jibu kwa mara nyingine (baada ya miaka 20
aliponidhihirishia kwa mara ya kwanza) la kwa nini nilizaliwa na nini
natakiwa kufanya.
Tuzo
ya Kiswahili ya Mabati-Cornell ya Fasihi ya Kiafrika, Kampuni ya Mabati
Rolling Mills ya Kenya, Kampuni ya Uchapishaji wa Vitabu ya Kwani Trust
ya Kenya na watu wote waliohudhulia sherehe ya tuzo hii katika ukumbi
wa Klabu ya Capital ya Nairobi. Ningependa kuwashukuru hao kwa
kukifanikisha kitu hiki, kwa ufadhili wao, kwa uenyeji wao na kwa kuacha
shughuli zao kuja kutushuhudia sisi tukipata tuzo zetu kwa mpangilio
huo.
Ningependa
pia kuwashukuru wale wote waliochaguliwa na Mungu kunifikisha katika
mafanikio haya ya Tuzo ya Mabati-Cornell; akiwemo Nyamuyengi Maregesi,
Amos Nungu na Beredy Malegesi kwa urafiki wao wa kweli.
Mwisho
kabisa ningependa kumshukuru bibi yangu, Martha Maregesi, aliyefariki
siku 18 kabla ya kutangazwa rasmi kwa tuzo hii huko Nijeria (tarehe 22
Novemba 2014) katika tamasha la vitabu la Ake Arts & Book Festival
la Abeokuta, kwa kunifundisha upendo kwa watu na uvumilivu katika
maisha. Tuzo hii ni kwa ajili ya bibi yangu. Asanteni sana.
No comments:
Post a Comment