Siku
 ya Alhamisi tarehe 3 Desemba 2015 nilipokea rasmi tuzo yangu ya 
Mabati-Cornell ya Fasihi ya Kiafrika jijini Nairobi nikiwa na washindi 
wenzangu Anna Samwel Manyanza, Mohammed Khelef Ghassani na Christopher 
Bundala Budebah. Hiki ni kitu kikubwa sana kutokea katika maisha yangu ya uandishi wa vitabu.
Awali
 ya yote ningependa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunifikisha siku hiyo 
na kunidhihirishia jibu kwa mara nyingine (baada ya miaka 20 
aliponidhihirishia kwa mara ya kwanza) la kwa nini nilizaliwa na nini 
natakiwa kufanya.
Tuzo
 ya Kiswahili ya Mabati-Cornell ya Fasihi ya Kiafrika, Kampuni ya Mabati
 Rolling Mills ya Kenya, Kampuni ya Uchapishaji wa Vitabu ya Kwani Trust
 ya Kenya na watu wote waliohudhulia sherehe ya tuzo hii katika ukumbi 
wa Klabu ya Capital ya Nairobi. Ningependa kuwashukuru hao kwa 
kukifanikisha kitu hiki, kwa ufadhili wao, kwa uenyeji wao na kwa kuacha
 shughuli zao kuja kutushuhudia sisi tukipata tuzo zetu kwa mpangilio 
huo.
Ningependa
 pia kuwashukuru wale wote waliochaguliwa na Mungu kunifikisha katika 
mafanikio haya ya Tuzo ya Mabati-Cornell; akiwemo Nyamuyengi Maregesi, 
Amos Nungu na Beredy Malegesi kwa urafiki wao wa kweli.
Mwisho
 kabisa ningependa kumshukuru bibi yangu, Martha Maregesi, aliyefariki 
siku 18 kabla ya kutangazwa rasmi kwa tuzo hii huko Nijeria (tarehe 22 
Novemba 2014) katika tamasha la vitabu la Ake Arts & Book Festival 
la Abeokuta, kwa kunifundisha upendo kwa watu na uvumilivu katika 
maisha. Tuzo hii ni kwa ajili ya bibi yangu. Asanteni sana.

No comments:
Post a Comment