Monday 16 April 2018

Swali la Tatizo ni Jibu la Tatizo

273. Jibu la tatizo hupatikana baada ya kujua swali la tatizo. Swali la tatizo ni jibu la tatizo. Si jibu la matokeo ya tatizo.

Kama tatizo ni ukame hutapata jibu la tatizo hilo mpaka ujue kwa nini kuna ukame. Inawezekana sababu ni mvua; inawezekana sababu ni migogoro ya ardhi au vita; inawezekana sababu ni ukataji miti ovyo; inawezekana sababu ni ardhi kukosa unyevunyevu kutokana na kupungua kwa vina vya mito; inawezekana sababu ni madhara ya ongezeko la joto duniani. Vyovyote itakavyokuwa, jibu litapatikana baada ya kujua chanzo cha tatizo.

Swali la tatizo ni kama vile, “Kwa nini moyo umepanuka?” Swali hilo linahitaji jibu sahihi. Inawezekana moyo umepanuka kutokana na figo kufeli, hivyo kushindwa kuchuja maji vizuri, na kwa sababu hiyo maji mengi kurudi kwenye moyo, hivyo kusababisha upanuke, kwa kusababishwa na wingi wa maji kwenye moyo. Kwa hiyo, badala ya kutibu moyo ambao ni matokeo ya tatizo, unatibu figo ambacho chanzo.

Swali la tatizo ni swali linaloulizia chanzo cha tatizo, litakaloleteleza ufumbuzi wa kudumu wa tatizo lenyewe.

Kwa hiyo, kwa kifupi: Jibu la tatizo hupatikana baada ya kujua chanzo sahihi cha tatizo, na kulitatua tatizo lenyewe.

No comments:

Post a Comment

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...