Monday 19 June 2017

Neema ya Mwenyezi Mungu


230. CV yako si maisha yako. Shahada yako si maisha yako. Maisha ni magumu kuliko mtu yeyote anavyoweza kufikiria.

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe anasemekana kuwa rais msomi zaidi kuliko wote duniani. Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini anasemekana kuwa rais asiye msomi zaidi kuliko wote duniani. Lakini wote ni marais wa nchi. Kusoma sana si kubaya, lakini hakuna mtu atakayefanikiwa katika maisha yake mpaka Mungu aamue. Mafanikio katika maisha hayategemei umesoma mpaka wapi, mafanikio katika maisha yanategemea neema ya Mwenyezi Mungu.

Kukosa elimu lisiwe jambo la kukukatisha tamaa; kukosa elimu si mwisho wa maisha. Mike Kidima alisema, “Nakata tamaa kukata tamaa.” Usikate tamaa, hata pale utakapokuwa umechoka, kabisa. Usitarajie kabisa kukata tamaa katika maisha, utakapokata utakata baraka.

1 comment:

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...