Monday 15 July 2013

Kitalifa

41. Ukitaka kuwa mfanyabiashara mzuri wa madawa ya kulevya usitumie madawa ya kulevya. Siri ya mafanikio ya Kolonia Santita ni nidhamu na kitalifa.

http//www.facebook.com/koloniasantita

4 comments:

  1. Kitalifa ni utiifu kamili, woga, umbali (kwa maana ya kuwa mbali na biashara ya mamafia wengine mpaka kwa makubaliano maalumu) na nidhamu ya kutoshirikiana na mamlaka zote za serikali. Ukishtakiwa kwa kosa la madawa au ujambazi ambalo hukufanya, utatumikia kifungo mpaka mwisho bila kushirikiana na polisi (kwa maana ya kutaja aliyehusika au waliohusika na uhalifu huo) hata kama aliyehusika au waliohusika hana au hawana uhusiano wowote na Kolonia Santita. Falsafa ya Kitalifa ni Sheria ya Kitalifa ya Kiapo cha Swastika cha Kolonia Santita. Na adhabu ya kuvunja sheria hiyo ni kifo – Kamusi ya Enock Maregesi.

    ReplyDelete
  2. Sichochei ufanyaji biashara ya madawa ya kulevya au halafa ya aina yoyote ile. Dhumuni la Falsafa ya Kitalifa ni burudani.

    ReplyDelete
  3. Ukitaka kuwa mfanyabiashara mzuri wa duka usinunue vitu dukani kwako,lazima uwe na discipline.

    ReplyDelete
  4. nidhamu ni msingi wa mafanikio

    ReplyDelete

Roho Yako

289. Roho yako inatoka wapi? Ya kwangu inatoka Tanzania. Kwa sababu amani na utulivu ndivyo vitu vya muhimu zaidi katika maisha yangu. ...